2 Nyakati 29 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version

2 Nyakati 29:1-36

Hezekia Mfalme Wa Yuda

(2 Wafalme 18:1-12)

129:1 1Nya 3:13; 2Nya 26:5; 2Fal 18:1Hezekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka ishirini na tisa. Mama yake aliitwa Abiya binti Zekaria. 229:2 2Nya 28:1; 34:2Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana kama Daudi baba yake alivyofanya.

329:3 2Fal 18:16; 2Nya 28:24; Mit 8:17Katika mwezi wa kwanza wa mwaka wa kwanza wa utawala wa alifungua milango ya Hekalu la Bwana, na kuikarabati. 4Akawaingiza makuhani na Walawi ndani na kuwakutanisha katika uwanja upande wa mashariki 529:5 Law 11:44; Neh 13:9; Efe 5:26-27; 1Nya 15:12; 2Nya 35:6; Eze 36:25; Mt 21:12-13; 1Kor 3:16-17; 2Kor 6:16na kusema: “Nisikilizeni mimi, enyi Walawi! Jitakaseni nafsi zenu sasa, mkaitakase na nyumba ya Bwana, Mungu wa baba zenu. Ondoeni uchafu wote kutoka mahali patakatifu. 629:6 Eze 23:35; Dan 9:5-6; 1Nya 5:25; Eze 8:16; Yer 2:27Baba zetu hawakuwa waaminifu, walifanya maovu machoni pa Bwana Mungu wetu na wakamwacha yeye. Wakageuza nyuso zao mbali na Maskani ya Bwana wakamgeuzia visogo vyao. 729:7 2Fal 16:17-18; 2Nya 28:24Pia walifunga milango ya ukumbi wa Hekalu na kuzima taa zake. Hawakufukiza uvumba wala kutoa sadaka yoyote ya kuteketezwa katika mahali patakatifu kwa Mungu wa Israeli. 829:8 Kum 28:25; 2Nya 24:18; Law 26:32; Eze 8:16; Yer 18:16; 1Fal 9:8; Yer 19:8; 29:18Kwa hiyo, hasira ya Bwana ikashuka juu ya Yuda na Yerusalemu, naye akawa amewafanya kitu cha kutisha, cha kushangaza na kitu cha kufanyia mzaha kama mnavyoona kwa macho yenu wenyewe. 929:9 2Nya 28:5-8, 17; Law 26:17Hii ndiyo sababu baba zetu wameanguka kwa upanga na ndiyo sababu wana wetu na binti zetu, pia wake zetu wamekuwa mateka. 1029:10 2Fal 11:17; 2Nya 15:12; Neh 9:38; Ezr 10:3; 2Nya 23:16Sasa ninadhamiria moyoni mwangu kuweka Agano na Bwana, Mungu wa Israeli, ili hasira yake kali igeuziwe mbali nasi. 1129:11 Hes 3:6; 8:6-14; 1Nya 15:2; 1Kor 6:9Wanangu, basi msipuuze jambo hili sasa, kwa kuwa Bwana amewachagua ninyi msimame mbele zake na kumtumikia, mkawe watumishi wake na mkamfukizie uvumba.”

1229:12 Hes 3:17-20; 2Nya 31:15Ndipo Walawi wafuatao wakaanza kazi:

Kutoka kwa Wakohathi,

Mahathi mwana wa Amasai na Yoeli mwana wa Azaria;

kutoka kwa Wamerari,

Kishi mwana wa Abdi na Azaria mwana wa Yahaleleli;

kutoka kwa Wagershoni,

Yoa mwana wa Zima na Edeni mwana wa Yoa;

1329:13 1Nya 6:36kutoka kwa wana wa Elisafani,

Shimri na Yeieli;

kutoka kwa wana wa Asafu,

Zekaria na Matania;

14kutoka kwa wana wa Hemani,

Yehieli na Shimei;

kutoka kwa wana wa Yeduthuni,

Shemaya na Uzieli.

1529:15 1Nya 23:28; Isa 1:25; 2Nya 30:12Walipomaliza kuwakusanya ndugu zao na kujiweka wakfu, wakaingia ndani ili kutakasa Hekalu la Bwana, kama vile mfalme alivyokuwa ameagiza, kwa kufuata neno la Bwana. 1629:16 2Sam 15:23Makuhani wakaingia patakatifu pa Hekalu la Bwana ili kupatakasa. Wakatoa nje penye ua wa Hekalu la Mungu kila kitu kichafu walichokikuta kwenye Hekalu la Bwana. Walawi wakavichukua na kuvipeleka nje katika Bonde la Kidroni. 1729:17 1Fal 6:3Walianza kazi ya utakaso siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza na kufikia siku ya nane ya mwezi huo wakawa wamefikia kwenye ukumbi wa Bwana. Kwa siku zingine nane wakalitakasa Hekalu lenyewe la Bwana wakakamilisha katika siku ya kumi na sita ya mwezi huo wa kwanza.

18Kisha wakaingia ndani kwa Mfalme Hezekia kutoa habari na kusema: “Tumelitakasa Hekalu lote la Bwana, madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa pamoja na vyombo vyake vyote, meza ya kupanga mikate iliyowekwa wakfu, pamoja na vyombo vyake vyote. 1929:19 2Nya 28:24Tumeviandaa na kuvitakasa vyombo vyote vile ambavyo Mfalme Ahazi, kwa kukosa uaminifu kwake, aliviondoa wakati alipokuwa mfalme. Sasa viko mbele ya madhabahu ya Bwana.”

Ibada Hekaluni Yarejeshwa

20Ndipo Mfalme Hezekia akainuka asubuhi na mapema, akakusanya pamoja maafisa wa mji wakakwea hekaluni mwa Bwana. 2129:21 Law 4:13-14Wakaleta mafahali saba, kondoo dume saba, wana-kondoo dume saba na mabeberu saba kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili ya ufalme, kwa ajili ya mahali patakatifu na kwa ajili ya Yuda. Mfalme akawaamuru makuhani, wazao wa Aroni, kuvitoa vitu hivyo sadaka katika madhabahu ya Bwana. 2229:22 Law 4:18; Hes 18:17; Ebr 9:21; Law 8:14-24Hivyo wakachinja wale mafahali, nao makuhani wakachukua ile damu na kuinyunyiza kwenye madhabahu, halafu wakawachinja wale kondoo dume saba na kunyunyiza hiyo damu yao kwenye madhabahu, kisha wakawachinja wale wana-kondoo dume na kunyunyiza damu yao kwenye madhabahu. 2329:23 Law 4:15, 24Wale mabeberu waliokuwa kwa ajili ya sadaka ya dhambi wakaletwa mbele ya mfalme na kusanyiko nao wakaweka mikono yao juu hao mabeberu. 2429:24 Kut 29:36; Law 4:20-26; Kol 1:20Ndipo makuhani wakawachinja hao mabeberu na kuweka damu yao kwenye madhabahu kwa ajili ya sadaka ya dhambi ili kufanya upatanisho kwa ajili ya Israeli yote, kwa sababu mfalme alikuwa ameamuru hiyo sadaka ya kuteketezwa na hiyo sadaka ya dhambi kwa ajili ya Israeli yote.

2529:25 1Nya 28:19; 2Nya 8:14; 1Sam 22:5; 2Sam 24:11; 1Nya 16:4; 23:6; 25:6; 2Nya 30:12Akawaweka Walawi kwenye Hekalu la Bwana wakiwa na matoazi, vinubi na zeze kama ilivyoagizwa na Daudi na Gadi mwonaji wa mfalme pamoja na nabii Nathani kwani hili lilikuwa limeamriwa na Bwana kupitia manabii wake. 2629:26 1Nya 15:16-24; 23:5; Hes 10:10; 2Nya 12:13; Amo 6:5; 1Nya 16:6Hivyo Walawi wakasimama tayari wakiwa na ala za uimbaji za Daudi na makuhani walikuwa na tarumbeta zao.

2729:27 1Sam 16:16; 2Nya 23:18; 20:21Hezekia akatoa amri ya kutoa sadaka ya kuteketezwa madhabahuni. Walipoanza kutoa sadaka, wakaanza pia kumwimbia Bwana pamoja na tarumbeta na zile ala za uimbaji za Daudi mfalme wa Israeli. 28Kusanyiko lote wakaabudu kwa kusujudu, wakati waimbaji wakiwa wanaimba na wenye tarumbeta wakipiga tarumbeta zao. Yote haya yaliendelea mpaka walipomaliza kutoa ile dhabihu ya sadaka ya kuteketezwa.

2929:29 2Nya 20:18; Rum 14:11Kutoa sadaka kulipomalizika, mfalme na kila mtu aliyekuwepo pamoja naye wakapiga magoti na kuabudu. 3029:30 Za 32:11; Flp 4:4Mfalme Hezekia na maafisa wake wakawaamuru Walawi kumsifu Bwana kwa maneno ya Daudi na ya Asafu mwonaji. Hivyo wakaimba sifa kwa furaha nao wakainamisha vichwa vyao na kuabudu.

3129:31 Ebr 13:15-16; Kut 35:22; 25:2; Law 7:12; 2Nya 13:9Kisha Hezekia akasema, “Sasa mmejiweka wakfu kwa Bwana. Njooni mlete dhabihu na sadaka za shukrani Hekaluni mwa Bwana.” Hivyo kusanyiko likaleta dhabihu na sadaka za shukrani, nao wote waliokuwa na mioyo ya hiari wakaleta sadaka za kuteketezwa.

32Idadi ya sadaka za kuteketezwa zilizoletwa na kusanyiko zilikuwa mafahali sabini, kondoo dume 100 na wana-kondoo dume 200. Wote hawa walikuwa kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kwa Bwana. 33Wanyama waliowekwa wakfu kwa sadaka ya kuteketezwa walikuwa mafahali 600, pamoja na kondoo na mbuzi 3,000. 3429:34 2Nya 35:11; Hes 8:15; 2Nya 30:3; Eze 44:11; 1Nya 29:17; Za 7:10Lakini makuhani walikuwa wachache sana kuweza kuchuna wale wanyama wote wa sadaka za kuteketezwa, kwa hiyo ndugu zao Walawi wakawasaidia mpaka kazi ile ikakamilika na mpaka makuhani wengine walipowekwa wakfu, kwa kuwa Walawi walikuwa makini kujiweka wakfu kuliko walivyokuwa makuhani. 3529:35 Mwa 4:4; 35:14; Hes 15:5-10; Law 3:16; 7:11-21; Kut 29:13Kulikuwa na sadaka nyingi za kuteketezwa, pamoja na mafuta ya wanyama ya sadaka za amani na sadaka za kinywaji ambazo ziliambatana na sadaka za kuteketezwa.

Kwa hiyo huduma ya Hekalu la Bwana ikarudishwa kwa upya. 3629:36 Za 118:23; Mdo 2:41Hezekia pamoja na watu wote wakafurahi kwa sababu ya lile Mungu alilolifanya kwa ajili ya watu wake, kwa kuwa lilitendeka papo hapo.

New International Version

2 Chronicles 29:1-36

Hezekiah Purifies the Temple

1Hezekiah was twenty-five years old when he became king, and he reigned in Jerusalem twenty-nine years. His mother’s name was Abijah daughter of Zechariah. 2He did what was right in the eyes of the Lord, just as his father David had done.

3In the first month of the first year of his reign, he opened the doors of the temple of the Lord and repaired them. 4He brought in the priests and the Levites, assembled them in the square on the east side 5and said: “Listen to me, Levites! Consecrate yourselves now and consecrate the temple of the Lord, the God of your ancestors. Remove all defilement from the sanctuary. 6Our parents were unfaithful; they did evil in the eyes of the Lord our God and forsook him. They turned their faces away from the Lord’s dwelling place and turned their backs on him. 7They also shut the doors of the portico and put out the lamps. They did not burn incense or present any burnt offerings at the sanctuary to the God of Israel. 8Therefore, the anger of the Lord has fallen on Judah and Jerusalem; he has made them an object of dread and horror and scorn, as you can see with your own eyes. 9This is why our fathers have fallen by the sword and why our sons and daughters and our wives are in captivity. 10Now I intend to make a covenant with the Lord, the God of Israel, so that his fierce anger will turn away from us. 11My sons, do not be negligent now, for the Lord has chosen you to stand before him and serve him, to minister before him and to burn incense.”

12Then these Levites set to work:

from the Kohathites,

Mahath son of Amasai and Joel son of Azariah;

from the Merarites,

Kish son of Abdi and Azariah son of Jehallelel;

from the Gershonites,

Joah son of Zimmah and Eden son of Joah;

13from the descendants of Elizaphan,

Shimri and Jeiel;

from the descendants of Asaph,

Zechariah and Mattaniah;

14from the descendants of Heman,

Jehiel and Shimei;

from the descendants of Jeduthun,

Shemaiah and Uzziel.

15When they had assembled their fellow Levites and consecrated themselves, they went in to purify the temple of the Lord, as the king had ordered, following the word of the Lord. 16The priests went into the sanctuary of the Lord to purify it. They brought out to the courtyard of the Lord’s temple everything unclean that they found in the temple of the Lord. The Levites took it and carried it out to the Kidron Valley. 17They began the consecration on the first day of the first month, and by the eighth day of the month they reached the portico of the Lord. For eight more days they consecrated the temple of the Lord itself, finishing on the sixteenth day of the first month.

18Then they went in to King Hezekiah and reported: “We have purified the entire temple of the Lord, the altar of burnt offering with all its utensils, and the table for setting out the consecrated bread, with all its articles. 19We have prepared and consecrated all the articles that King Ahaz removed in his unfaithfulness while he was king. They are now in front of the Lord’s altar.”

20Early the next morning King Hezekiah gathered the city officials together and went up to the temple of the Lord. 21They brought seven bulls, seven rams, seven male lambs and seven male goats as a sin offering29:21 Or purification offering; also in verses 23 and 24 for the kingdom, for the sanctuary and for Judah. The king commanded the priests, the descendants of Aaron, to offer these on the altar of the Lord. 22So they slaughtered the bulls, and the priests took the blood and splashed it against the altar; next they slaughtered the rams and splashed their blood against the altar; then they slaughtered the lambs and splashed their blood against the altar. 23The goats for the sin offering were brought before the king and the assembly, and they laid their hands on them. 24The priests then slaughtered the goats and presented their blood on the altar for a sin offering to atone for all Israel, because the king had ordered the burnt offering and the sin offering for all Israel.

25He stationed the Levites in the temple of the Lord with cymbals, harps and lyres in the way prescribed by David and Gad the king’s seer and Nathan the prophet; this was commanded by the Lord through his prophets. 26So the Levites stood ready with David’s instruments, and the priests with their trumpets.

27Hezekiah gave the order to sacrifice the burnt offering on the altar. As the offering began, singing to the Lord began also, accompanied by trumpets and the instruments of David king of Israel. 28The whole assembly bowed in worship, while the musicians played and the trumpets sounded. All this continued until the sacrifice of the burnt offering was completed.

29When the offerings were finished, the king and everyone present with him knelt down and worshiped. 30King Hezekiah and his officials ordered the Levites to praise the Lord with the words of David and of Asaph the seer. So they sang praises with gladness and bowed down and worshiped.

31Then Hezekiah said, “You have now dedicated yourselves to the Lord. Come and bring sacrifices and thank offerings to the temple of the Lord.” So the assembly brought sacrifices and thank offerings, and all whose hearts were willing brought burnt offerings.

32The number of burnt offerings the assembly brought was seventy bulls, a hundred rams and two hundred male lambs—all of them for burnt offerings to the Lord. 33The animals consecrated as sacrifices amounted to six hundred bulls and three thousand sheep and goats. 34The priests, however, were too few to skin all the burnt offerings; so their relatives the Levites helped them until the task was finished and until other priests had been consecrated, for the Levites had been more conscientious in consecrating themselves than the priests had been. 35There were burnt offerings in abundance, together with the fat of the fellowship offerings and the drink offerings that accompanied the burnt offerings.

So the service of the temple of the Lord was reestablished. 36Hezekiah and all the people rejoiced at what God had brought about for his people, because it was done so quickly.