1 Wafalme 16 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

1 Wafalme 16:1-34

116:1 1Fal 16:7; 2Nya 19:2Ndipo neno la Bwana likamjia Yehu mwana wa Hanani dhidi ya Baasha, kusema: 216:2 1Fal 14:7-9“Nilikuinua kutoka mavumbini na kukufanya kiongozi wa watu wangu Israeli, lakini ukaenenda katika njia za Yeroboamu na kusababisha watu wangu Israeli kutenda dhambi na kunikasirisha kwa dhambi zao. 316:3 1Fal 16:11; 21:22Basi nitamwangamiza Baasha pamoja na nyumba yake, nami nitaifanya nyumba yako kama ile ya Yeroboamu mwanawe Nebati. 416:4 1Fal 14:11Mbwa watawala watu wa Baasha watakaofia mjini na ndege wa angani watajilisha kwa wale watakaofia mashambani.”

5Kwa matukio mengine ya utawala wa Baasha, aliyoyafanya na mafanikio yake, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli? 6Baasha akalala na baba zake naye akazikwa huko Tirsa. Naye Ela mwanawe akawa mfalme baada yake.

716:7 1Fal 16:11Zaidi ya hayo, neno la Bwana likamjia Baasha pamoja na nyumba yake kupitia kwa nabii Yehu mwana wa Hanani, kwa sababu ya maovu yote aliyokuwa ametenda machoni pa Bwana, akamkasirisha kwa mambo aliyotenda, na kuwa kama nyumba ya Yeroboamu, na pia kwa sababu aliiangamiza.

Ela Mfalme Wa Israeli

8Katika mwaka wa ishirini na sita wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Ela mwana wa Baasha akawa mfalme wa Israeli, naye akatawala huko Tirsa kwa miaka miwili.

916:9 1Fal 20:12; Mit 31:4-5Zimri, mmoja wa maafisa wake, aliyekuwa na amri juu ya nusu ya magari yake ya vita, akafanya hila mbaya dhidi ya Ela. Wakati huo Ela alikuwa Tirsa, akilewa katika nyumba ya Arsa, mtu aliyekuwa msimamizi wa jumba la kifalme huko Tirsa. 1016:10 2Fal 9:31Zimri akaingia, akampiga na kumuua katika mwaka wa ishirini na saba wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda. Kisha Zimri akaingia mahali pake kuwa mfalme.

11Mara tu alipoanza kutawala na kuketi juu ya kiti cha ufalme, aliua jamaa yote ya Baasha. Hakumwacha mwanaume hata mmoja, akiwa ni ndugu au rafiki. 12Hivyo Zimri akaangamiza jamaa yote ya Baasha, kulingana na neno la Bwana lililonenwa dhidi ya Baasha kupitia nabii Yehu: 1316:13 Kum 32:21kwa sababu ya dhambi zote Baasha na mwanawe Ela walizokuwa wametenda na wakasababisha Israeli kuzitenda, basi wakamkasirisha Bwana, Mungu wa Israeli kwa sanamu zao zisizofaa.

14Kwa matukio mengine ya utawala wa Ela, na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?

Zimri Mfalme Wa Israeli

1516:15 Yos 19:44Katika mwaka wa ishirini na saba wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Zimri akatawala huko Tirsa siku saba. Jeshi lilikuwa limepiga kambi karibu na Gibethoni, mji wa Wafilisti. 16Wakati Waisraeli waliokuwa kambini waliposikia kuwa Zimri alikuwa amefanya hila mbaya dhidi ya mfalme na kumuua, wakamtangaza Omri, jemadari wa jeshi, kuwa mfalme wa Israeli siku iyo hiyo huko kambini. 17Ndipo Omri na Waisraeli wote pamoja naye wakaondoka Gibethoni na kuizingira Tirsa. 18Wakati Zimri alipoona kuwa mji umechukuliwa, alikwenda ndani ya ngome ya jumba la kifalme na kulichoma moto jumba la kifalme na kujiteketeza ndani yake. Kwa hiyo akafa, 19kwa sababu ya dhambi alizofanya, akitenda maovu machoni pa Bwana na kuenenda katika njia za Yeroboamu na katika dhambi alizofanya na kusababisha Israeli kuzifanya.

20Kwa matukio mengine ya utawala wa Zimri, na uasi alioutenda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?

Omri Mfalme Wa Israeli

21Ndipo watu wa Israeli wakagawanyika katika makundi mawili, nusu wakamuunga mkono Tibni mwana wa Ginathi ili awe mfalme na nusu nyingine wakamuunga mkono Omri. 22Lakini wafuasi wa Omri wakajionyesha wenye nguvu kuliko wale wa Tibni mwana wa Ginathi. Hivyo Tibni akafa na Omri akawa mfalme.

2316:23 Yos 12:24Katika mwaka wa thelathini na moja wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Omri akawa mfalme wa Israeli, naye akatawala kwa miaka kumi na miwili, sita kati ya hiyo katika Tirsa. 2416:24 1Fal 13:32; Mt 10:5Alinunua kilima cha Samaria kutoka kwa Shemeri kwa talanta mbili16:24 Talanta mbili za fedha ni sawa na kilo 70. za fedha na akajenga mji juu ya hicho kilima, akiuita Samaria, kutokana na Shemeri, jina la mmiliki wa kwanza wa kilima hicho.

2516:25 Kum 4:25; Mik 6:16Lakini Omri akatenda maovu machoni pa Bwana na kutenda dhambi kuliko wote waliomtangulia. 2616:26 Kum 32:21Akaenenda katika njia zote za Yeroboamu mwana wa Nebati na katika dhambi zake, ambazo alisababisha Israeli kutenda, hivyo basi wakamkasirisha Bwana, Mungu wa Israeli kwa sanamu zao zisizofaa.

27Kwa matukio mengine ya utawala wa Omri, yale aliyofanya na vitu alivyovifanikisha, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli? 2816:28 1Fal 13:32Omri akalala pamoja na baba zake na akazikwa huko Samaria. Ahabu mwanawe akatawala mahali pake.

Ahabu Afanywa Mfalme Wa Israeli

29Katika mwaka wa thelathini na nane wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Ahabu mwana wa Omri akawa mfalme wa Israeli, naye akatawala Israeli akiwa Samaria kwa miaka ishirini na miwili. 3016:30 1Fal 14:9Ahabu mwana wa Omri akafanya maovu zaidi machoni mwa Bwana kuliko yeyote aliyewatangulia. 3116:31 1Fal 11:2; 2Fal 9:34; Amu 3:6Kama vile haikutosha kuishi kama Yeroboamu mwana wa Nebati, akamwoa Yezebeli binti wa Ethbaali, mfalme wa Wasidoni, naye akaanza kumtumikia Baali na kumwabudu. 3216:32 Amu 6:28; Yer 43:12Akajenga madhabahu kwa ajili ya Baali katika hekalu la Baali lile alilolijenga huko Samaria. 3316:33 Amu 3:7; 2Fal 13:6Pia Ahabu akatengeneza nguzo ya Ashera na kufanya mengi ili kumkasirisha Bwana, Mungu wa Israeli, kuliko walivyofanya wafalme wote wa Israeli waliomtangulia.

3416:34 Yos 6:26Katika wakati wa Ahabu, Hieli, Mbetheli, akaijenga upya Yeriko. Aliweka misingi yake kwa gharama ya mzaliwa wake wa kwanza Abiramu, na kuweka malango yake kwa gharama ya mwanawe mdogo Segubu, kulingana na neno la Bwana alilosema kupitia Yoshua mwana wa Nuni.

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

列王紀上 16:1-34

1耶和華吩咐哈拿尼的兒子耶戶先知責備巴沙說: 2「我從塵土中提拔你,立你為我以色列子民的首領,你卻重蹈耶羅波安的覆轍,使我的子民陷入罪中,惹我發怒。 3所以我必除掉你和你全家,像除掉尼八的兒子耶羅波安家一樣。 4你家人中,死在城中的必被狗吃,死在野外的必被鳥吃。」

5巴沙其他的事蹟和功業都記在《以色列列王史》上。 6巴沙與祖先同眠後葬在得撒,他兒子以拉繼位。 7耶和華藉哈拿尼的兒子耶戶先知譴責巴沙和他全家,是因為他像耶羅波安家一樣做耶和華視為惡的事,惹耶和華發怒,也因為他殺了耶羅波安全家。

以拉做以色列王

8猶大亞撒執政第二十六年,巴沙的兒子以拉得撒登基做以色列王,執政兩年。 9以拉的一半戰車由部下心利掌管。心利卻背叛他,趁他在得撒宮廷總管亞雜家中喝醉時, 10進去殺了他,篡了位。那一年是亞撒猶大王第二十七年。

11心利一登基做王,就殺了巴沙全家,他親友家的男子也無一倖免。 12巴沙慘遭滅門之禍,正應驗了耶和華藉耶戶先知譴責他的話。 13這是因為巴沙以拉父子二人作惡多端,祭拜假神,使以色列人陷入罪中,惹以色列的上帝耶和華發怒。 14以拉其他的事及一切所為都記在《以色列列王史》上。

心利做以色列王

15猶大亞撒執政第二十七年,心利開始在得撒做王,執政僅七天。那時以色列軍正在攻打非利士基比頓城。 16他們聽說心利謀反弒君,就在當天擁立軍中元帥暗利以色列王。 17暗利率領以色列軍離開基比頓,上去圍攻得撒18心利見城被攻破,就走進王宮的城堡中放火燒宮,自焚而死。 19這是因為他犯罪,行耶和華視為惡的事,步耶羅波安的後塵,使以色列人陷入罪中。 20心利其他的事及其謀反篡位的經過,都記在《以色列列王史》上。

暗利做以色列王

21那時,以色列人分為兩派,一派擁立基納的兒子提比尼做王,另一派支持暗利22暗利一派強於提比尼一派。提比尼死後,暗利做了王。

23猶大亞撒執政第三十一年,暗利登基做以色列王,執政共十二年,其中六年在得撒24暗利用了一千四百兩銀子向撒瑪買了撒瑪利亞山,在上面建了一座城,按原來主人撒瑪的名字稱之為撒瑪利亞25暗利做耶和華視為惡的事,比以前的諸王更壞。 26他步尼八的兒子耶羅波安的後塵,使以色列人陷入罪中,祭拜假神,惹以色列的上帝耶和華發怒。 27暗利其他的事及一切所為都記在《以色列列王史》上。 28暗利與祖先同眠後葬在撒瑪利亞,他兒子亞哈繼位。

亞哈做以色列王

29猶大亞撒執政第三十八年,暗利的兒子亞哈登基做以色列王,他在撒瑪利亞執政二十二年。 30暗利的兒子亞哈做耶和華視為惡的事,比以前的諸王更壞。 31他不但步尼八的兒子耶羅波安的後塵,還娶了西頓葉巴力的女兒耶洗別為妻,供奉、祭拜巴力32他在撒瑪利亞巴力建廟,在廟裡為巴力設立祭壇。 33他還造了亞舍拉神像,所作所為比先前諸王更惹以色列的上帝耶和華發怒。 34亞哈執政期間,伯特利希伊勒重建耶利哥城。他立地基的時候,長子亞比蘭死了;安城門的時候,幼子西割死了。這應驗了耶和華藉的兒子約書亞說的話。