1 Samweli 23 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version

1 Samweli 23:1-29

Daudi Aokoa Keila

123:1 Yos 15:44; Hes 18:27; Amu 6:11Daudi alipoambiwa kuwa, “Tazama, Wafilisti wanapigana dhidi ya Keila nao wanapokonya nafaka katika sakafu za kupuria,” 223:2 1Sam 22; 10; 30:8; 2:1; 2Sam 5:19; Za 50:19; Hes 27:21; Amu 1:1; 1Sam 28:6; 30:8; 1Nya 10:14; 14:10; Za 32:8; 37:5; Mit 3:5, 6; Yer 10:23; Yak 1:5akauliza kwa Bwana, akisema, “Je, niende na kuwashambulia hawa Wafilisti?”

Bwana akamjibu, “Nenda, washambulie Wafilisti na uuokoe Keila.”

3Lakini watu wa Daudi wakamwambia, “Hapa Yuda kwenyewe tunaogopa. Si zaidi sana, kama tukienda Keila dhidi ya majeshi ya Wafilisti!”

423:4 1Sam 9:16; Yos 8:7; Amu 7:7Daudi akauliza kwa Bwana tena, naye Bwana akamjibu akamwambia, “Shuka uende Keila, kwa kuwa nitawatia Wafilisti mkononi mwako.” 5Basi Daudi na watu wake wakaenda Keila, wakapigana na Wafilisti na kutwaa wanyama wao wa kutosha. Daudi akawatia hasara kubwa Wafilisti na kuwaokoa watu wa Keila. 623:6 1Sam 22:20; 2:28; Ay 1:15-19(Basi Abiathari mwana wa Ahimeleki alikuwa ameleta kisibau alipokimbilia kwa Daudi huko Keila.)

Sauli Anamfuata Daudi

723:7 Kum 32:30; Za 31:21; Kut 15:9; 1Sam 24:4-6; 26:8, 9; Za 79:11Sauli akaambiwa kwamba Daudi alikuwa amekwenda Keila, naye akasema, “Mungu amemtia mkononi mwangu, kwa kuwa Daudi amejifunga mwenyewe kwa kuingia kwenye mji wenye malango na makomeo.” 8Naye Sauli akayaita majeshi yake yote yaende vitani, kuishukia Keila ili kumzingira Daudi na watu wake kwa jeshi.

923:9 1Sam 22:20; 2:28; 30:7Daudi alipojua kuwa Sauli alikuwa ana hila dhidi yake, akamwambia Abiathari kuhani, “Leta kile kisibau.” 1023:10 1Sam 22:19; 2Sam 20:20; Es 3:6; Za 44:22Daudi akasema, “Ee Bwana, Mungu wa Israeli, mtumishi wako amesikia kwa hakika kwamba Sauli anapanga kuja Keila na kuangamiza mji kwa ajili yangu. 11Je, watu wa Keila watanisalimisha kwake? Je, Sauli atateremka, kama mtumishi wako alivyosikia? Ee Bwana, Mungu wa Israeli, mwambie mtumishi wako.”

Naye Bwana akasema, “Ndiyo, atashuka.”

12Daudi akauliza tena, “Je watu wa Keila watanisalimisha mimi pamoja na watu wangu kwa Sauli?”

Naye Bwana akasema, “Ndiyo, watafanya hivyo.”

1323:13 1Sam 22:2; 25:13Basi Daudi na watu wake, wapatao 600, wakaondoka Keila wakawa wanakwenda sehemu moja hadi nyingine. Sauli alipoambiwa Daudi ametoroka kutoka Keila, hakwenda huko.

1423:14 Za 55:7; Yos 15:24; Za 54:3-4; 32:7; 11:1; Yos 15:55; 1Sam 27:1; Mit 1:16; 4:16; Kum 33:3; 1Sam 2:9; Za 32:7; 33:18; Mit 2:8; Rum 8:31; 2Tim 3:11; 4:17, 18Daudi akakaa katika ngome za jangwani na katika vilima vya Jangwa la Zifu. Siku baada ya siku Sauli aliendelea kumsaka, lakini Mungu hakumtia Daudi mikononi mwake.

1523:15 1Sam 20:1Daudi alipokuwa huko Horeshi katika Jangwa la Zifu, akajua kuwa Sauli alikuwa amekuja ili amuue. 1623:16 1Sam 30:6; Za 18:2; 27:14Naye Yonathani mwana wa Sauli akamwendea Daudi huko Horeshi na kumtia moyo kusimama imara katika imani yake kwa Mungu. 1723:17 1Sam 20:31; 24:20Akamwambia, “Usiogope, Daudi; baba yangu Sauli hatakutia mkononi mwake. Utakuwa mfalme juu ya Israeli, nami nitakuwa wa pili wako. Hata baba yangu Sauli anajua hili.” 1823:18 1Sam 18:3; 2Sam 9:1; 21:7Wote wawili wakaweka agano mbele za Bwana. Kisha Yonathani akaenda zake nyumbani, lakini Daudi akabaki Horeshi.

1923:19 1Sam 26:1; Za 54; 1Sam 26:3Basi Wazifu wakakwea kwa Sauli huko Gibea na kusema, “Je, Daudi hajifichi miongoni mwetu katika ngome huko Horeshi, katika kilima cha Hakila, kusini mwa Yeshimoni? 20Sasa, ee mfalme, uteremke wakati wowote unapoona vyema kufanya hivyo, sisi tutawajibika kumkabidhi kwa mfalme.”

2123:21 Rut 2:20; 2Sam 2:5; 1Sam 22:8Sauli akajibu, “Bwana awabariki kwa kunifikiria. 22Nendeni mkafanye maandalizi zaidi. Mkajue mahali ambapo Daudi huenda mara kwa mara na nani amepata kumwona huko. Wananiambia yeye ni mwerevu sana. 2323:23 Mwa 31:36Jueni kila mahali anapojificha mrudi na kunipa taarifa kamili. Kisha nitakwenda pamoja nanyi; kama atakuwa katika eneo hilo, nitamsaka miongoni mwa koo zote za Yuda.”

2423:24 Yos 15:55; 1Sam 26:1; 25:2Basi wakaondoka na kwenda mpaka Zifu wakimtangulia Sauli. Naye Daudi na watu wake walikuwa katika Jangwa la Maoni, katika Araba kusini mwa Yeshimoni. 25Sauli na watu wake wakaanza msako, naye Daudi alipoelezwa hili, akateremka mpaka mwambani na kukaa katika Jangwa la Maoni. Sauli aliposikia hili, akaenda katika Jangwa la Maoni akimfuata Daudi.

2623:26 Za 17:6; 1Sam 19:12; 20:38; 2Sam 15:14; Za 31:22; 2Nya 20:12; 2Kor 1:8Sauli alikuwa akienda upande mmoja wa mlima, naye Daudi na watu wake walikuwa upande mwingine wa mlima, wakiharakisha kumkimbia Sauli. Wakati Sauli na majeshi yake walipokaribia kumkamata Daudi na watu wake, 2723:27 Kum 32:36; 1Sam 14:6; 2Sam 22:1-51; 2Fal 19:9; Za 18:1-50; Isa 37:6-9; 59:1; Yer 15:20, 21mjumbe alikuja kwa Sauli, akisema, “Njoo haraka! Wafilisti wanaishambulia nchi.” 28Ndipo Sauli akarudi akaacha kumfuata Daudi na kwenda kukabiliana na Wafilisti. Ndiyo sababu wanaiita sehemu hii Sela-Hamalekothi.23:28 Sela-Hamalekothi maana yake Mwamba wa Kutengana. 2923:29 1Sam 24:22; Yos 15:62; 2Nya 20:2; Wim 1:14Naye Daudi akakwea kutoka huko na kuishi katika ngome za En-Gedi.

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

撒母耳记上 23:1-29

大卫营救基伊拉

1一天,大卫得知非利士人正在攻打基伊拉,抢掠麦场, 2便求问耶和华:“我可以去攻打非利士人吗?”耶和华答道:“你可以去攻打非利士人,营救基伊拉。” 3大卫的部下却对他说:“我们在犹大这里尚且胆战心惊,何况去基伊拉攻打非利士军队呢!” 4大卫再求问耶和华,耶和华答道:“到基伊拉去吧,我一定把非利士人交在你手里。” 5于是,大卫和部下到基伊拉去攻打非利士人,大败敌人,夺取了他们的牲畜,救出基伊拉人。

6亚希米勒的儿子祭司亚比亚他基伊拉投奔大卫时,把以弗得也带了去。 7扫罗得知大卫基伊拉,就说:“这一次是上帝把他交在我手中了,因为他竟然自投网罗,进入有门有闩的城。” 8扫罗召集全军准备攻打基伊拉,围困大卫和他的部下。 9大卫知道了扫罗的计谋,便吩咐祭司亚比亚他把以弗得带来, 10然后说:“耶和华,以色列的上帝啊,仆人听说扫罗要来毁灭基伊拉城,因为我在这里。 11基伊拉的人会不会把我交给扫罗呢?扫罗是不是像我听说的那样要来这里呢?耶和华,以色列的上帝啊,求你告诉我。”耶和华说:“扫罗一定会来。” 12大卫又问耶和华:“基伊拉的人会不会把我和我的部下交给扫罗呢?”耶和华说:“他们一定会。” 13于是,大卫率领自己的六百部下离开基伊拉,到处流浪。扫罗得知大卫已经离开基伊拉,就不去了。

14大卫住在旷野的堡垒或西弗旷野的山区。扫罗天天搜捕大卫,但上帝没有把大卫交在他的手中。 15大卫西弗旷野的何利沙得知扫罗要来杀他。 16扫罗的儿子约拿单何利沙大卫,鼓励大卫坚定地信靠上帝。 17他对大卫说:“不要害怕,我父亲扫罗害不了你。你将做以色列的王,我将做你的宰相。我父亲也明白这一点。” 18二人在耶和华面前立了约。之后,大卫仍留在何利沙约拿单则回家去了。

19西弗人去基比亚扫罗,说:“大卫就躲在我们那里,在旷野南面哈基拉山上何利沙的堡垒里。 20王啊,你随时都可以下来,我们一定把他交在王的手里。” 21扫罗说:“愿耶和华赐福给你们!因为你们体恤我。 22我听说他非常狡猾,你们再回去弄清楚他的行踪及谁在那里见过他, 23查明他的藏身之处,回来如实告诉我,然后我会与你们同去。如果他在犹大境内,我要搜遍千家万户,找到他。” 24于是,西弗人先回去了。当时大卫和他的部下在旷野南面的亚拉巴,即玛云旷野。 25大卫听说扫罗和手下正在搜寻他,便率领部下前往玛云旷野的磐石,住在那里。扫罗得知后,便去玛云旷野追赶大卫26扫罗在山这边走,大卫和他的部下在山那边走,急急忙忙地躲避扫罗扫罗和他的手下四面包围过来,眼看就要抓住他们了。 27这时,扫罗的信使前来禀报,说非利士人前来犯境,请王速回。 28扫罗只好放弃追赶大卫,回师迎战非利士人。因此,那地方叫“脱险岩”。 29后来,大卫从那里转移到隐·基底的堡垒里。