1 Nyakati 16 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

1 Nyakati 16:1-43

Sanduku Lawekwa Ndani Ya Hema

116:1 2Sam 6:17-19Wakaleta Sanduku la Mungu na kuliweka ndani ya hema ambalo Daudi alikuwa amelisimamisha kwa ajili yake, na wakatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele za Mungu. 216:2 Kut 39:43; Hes 6:23-27Baada ya Daudi kumaliza kutoa hizo sadaka za kuteketezwa na hizo sadaka za amani, akawabariki watu katika jina la Bwana. 3Kisha akamgawia kila Mwisraeli mwanaume na mwanamke mkate, andazi la tende na andazi la zabibu kavu.

416:4 1Nya 15:1-2Akawaweka pia baadhi ya Walawi ili wahudumu mbele ya Sanduku la Bwana kufanya maombi, kumshukuru na kumsifu Bwana, Mungu wa Israeli: 5Asafu ndiye alikuwa mkuu wao, akisaidiwa na Zekaria, Yeieli, Shemiramothi, Yehieli, Matithia, Eliabu, Benaya, Obed-Edomu na Yeieli. Hawa ndio wangepiga zeze na vinubi, Asafu angepiga matoazi, 6nao Benaya na Yahazieli makuhani, ndio wangepiga tarumbeta mara kwa mara mbele ya Sanduku la Agano la Mungu.

Zaburi Ya Daudi Ya Shukrani

(Zaburi 105:1-15; 96:1-13; 106:1, 47-48)

716:7 2Sam 23:1; Za 47:7Siku ile, kitu cha kwanza Daudi alichofanya ni kumkabidhi Asafu na wenzake zaburi hii ya shukrani kwa Bwana:

816:8 Za 107:1; 118:1; 2Fal 19:19Mshukuruni Bwana, liitieni jina lake;

wajulisheni mataifa yale aliyoyatenda.

916:9 Za 100:1; Kut 15:1; Za 7:17; 95:1-2Mwimbieni yeye, mwimbieni yeye sifa;

waambieni matendo yake yote ya ajabu.

1016:10 Za 34:3; Isa 45:25Lishangilieni jina lake takatifu;

mioyo ya wale wamtafutao Bwana na ifurahi.

1116:11 Za 27:8; Mit 8:17; Amo 5:6-14Mtafuteni Bwana na nguvu zake;

utafuteni uso wake siku zote.

1216:12 Za 78:43; 103:2Kumbuka matendo ya ajabu aliyoyafanya,

miujiza yake na hukumu alizozitamka,

13enyi wazao wa Israeli mtumishi wake,

enyi wana wa Yakobo, wateule wake.

1416:14 Isa 29:9; 4:4Yeye ndiye Bwana Mungu wetu;

hukumu zake zimo duniani pote.

15Hulikumbuka agano lake milele,

neno ambalo aliamuru, kwa vizazi elfu,

1616:16 Mwa 17:2; Neh 9:8; Ebr 6:13-18; Za 105:8-10; Mwa 15:18; 26:3agano alilolifanya na Abrahamu,

kiapo alichomwapia Isaki.

1716:17 Mwa 35:9-12Alilithibitisha kwa Yakobo kuwa amri,

kwa Israeli liwe agano la milele:

1816:18 Mwa 13:14-17“Nitakupa wewe nchi ya Kanaani

kuwa sehemu utakayoirithi.”

1916:19 Mwa 34:30; Ebr 11:13; Kum 7:7Walipokuwa wachache kwa idadi,

wachache sana na wageni ndani yake,

20walitangatanga kutoka taifa moja hadi jingine,

kutoka ufalme mmoja hadi mwingine.

2116:21 Mwa 20:3; Kut 7:15-18; Za 9:5; Mwa 12:17Hakuruhusu mtu yeyote awaonee;

kwa ajili yao aliwakemea wafalme, akisema:

2216:22 Mwa 20:7; Za 105; 15; 1Yn 2:27“Msiwaguse niliowatia mafuta;

msiwadhuru manabii wangu.”

2316:23 Za 47:1; 96:1Mwimbieni Bwana dunia yote;

tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.

2416:24 Isa 12:4Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa,

matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.

2516:25 Za 18:3; 76:7; 89:7; Kut 18:11; Isa 40:25-26; Za 24:8Kwa kuwa Bwana ni mkuu,

mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote;

yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.

2616:26 Law 19:4; Isa 45:20; 1Kor 8:4; Za 115:4-8; Yer 10:3Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu,

lakini Bwana aliziumba mbingu.

27Fahari na enzi viko mbele yake;

nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.

2816:28 Za 29:1-2; 8:1Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa,

mpeni Bwana utukufu na nguvu,

29mpeni Bwana utukufu

unaostahili jina lake.

Leteni sadaka na mje katika nyua zake;

mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake.

3016:30 Za 2:11; 33:8Dunia yote na itetemeke mbele zake!

Ulimwengu ameuweka imara; hauwezi kusogezwa.

3116:31 Isa 44:23; 35:10; 49:13; Mao 5:19; Isa 52:7; Lk 2:13; Ufu 14:2Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi;

semeni katikati ya mataifa, “Bwana anatawala!”

3216:32 Kut 20:11; Za 98:7; 96:10Bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake;

mashamba na yashangilie, na vyote vilivyomo ndani yake.

3316:33 Isa 14:8; 55:12; Za 110:6Kisha miti ya msituni itaimba,

itaimba kwa furaha mbele za Bwana,

kwa maana anakuja kuihukumu dunia.

3416:34 Isa 12:4; Za 25:7; Ezr 3:11; Yer 33:1Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema;

upendo wake wadumu milele.

3516:35 Kum 32:15; Mik 7:7; Ezr 3:11; Yer 33:11; Za 106:47Mlilieni, “Ee Mungu Mwokozi wetu, tuokoe.

Tukusanye tena na utukomboe kutoka kwa mataifa,

ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu,

na kushangilia katika sifa zako.”

3616:36 Kum 27:15; 1Fal 8:15; Neh 8:6; 10:27; 2Nya 8:14; Za 72:18-19Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli,

tangu milele na hata milele.

Nao watu wote wakasema, “Amen,” na “Msifuni Bwana.”

37Daudi akamwacha Asafu na wenzake mbele ya Sanduku la Agano la Bwana ili wahudumu humo mara kwa mara, kulingana na mahitaji ya kila siku. 3816:38 1Nya 13:13; 26:4-10Pia akamwacha Obed-Edomu pamoja na wenzake sitini na wanane wahudumu pamoja nao. Obed-Edomu mwana wa Yeduthuni na pia Hosa walikuwa mabawabu wa lango.

3916:39 1Sam 2:35; 1Nya 21:29; 2Sam 8:17; Yos 9:3; 1Fal 3:4Daudi akamwacha kuhani Sadoki pamoja na makuhani wenzake mbele ya hema ya ibada ya Bwana katika mahali pa juu pa kuabudia huko Gibeoni 4016:40 Kut 29:38; Hes 28:1-8ili kutoa sadaka za kuteketezwa kwa Bwana kwenye madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa mara kwa mara, asubuhi na jioni, sawasawa na kila kitu kilichoandikwa katika sheria ya Bwana ambayo alikuwa amempa Israeli. 4116:41 1Nya 15:19; 2Nya 5:13; Yak 5:11; Ezr 3:11; Neh 9:17; Za 25:10; 33:5; Yer 33:11; Yoe 2:13; Lk 3:36Waliohudumu pamoja nao walikuwa Hemani, Yeduthuni na wale wote waliochaguliwa na kutajwa kwa jina kumpa Bwana shukrani, “Kwa maana fadhili zake zadumu milele.” 4216:42 2Nya 7:6Hemani na Yeduthuni walikuwa na wajibu wa kupiga tarumbeta, matoazi na kutumia vyombo vingine kwa ajili ya nyimbo za sifa kwa Mungu. Wana wa Yeduthuni waliwekwa langoni.

4316:43 2Sam 6:19-20; Mwa 18:19; Yos 24:15Kisha watu wote wakaondoka, kila mmoja akarudi nyumbani kwake, naye Daudi akarudi nyumbani kuibariki jamaa yake.

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

歷代志上 16:1-43

1眾人把上帝的約櫃抬進去,安放在大衛所搭的帳幕裡,然後在上帝面前獻上燔祭和平安祭。 2大衛獻上燔祭和平安祭後,就奉耶和華的名給民眾祝福, 3又給所有以色列人,不論男女,每人一個餅、一塊肉和一個葡萄餅。

4大衛指派一些利未人在耶和華的約櫃前事奉,頌揚、稱謝和讚美以色列的上帝耶和華。 5為首的是亞薩,其次是撒迦利雅雅薛示米拉末耶歇瑪他提雅以利押比拿雅俄別·以東耶利,他們鼓瑟彈琴,亞薩敲鈸。 6比拿雅雅哈悉兩位祭司在上帝的約櫃前吹號。

大衛的頌歌

7那一天,大衛初次指派亞薩和他的親族唱詩歌頌耶和華,說:

8「你們要稱謝耶和華,

呼求祂的名,

在列邦傳揚祂的作為。

9要歌頌、讚美祂,

述說祂一切奇妙的作為。

10要以祂的聖名為榮,

願尋求耶和華的人心中快樂。

11要尋求耶和華和祂的能力,

時常來到祂面前。

12-13祂僕人以色列的後裔啊,

祂所揀選的雅各的子孫啊,

要記住祂所行的神蹟奇事和祂口中的判詞。

14「祂是我們的上帝耶和華,

祂在普天下施行審判。

15要永遠銘記祂的約,

歷經千代也不可忘記祂的應許,

16就是祂與亞伯拉罕所立的約,

以撒所起的誓。

17祂將這約定為律例賜給雅各

定為永遠的約賜給以色列

18祂說,『我必把迦南賜給你,

作為你的產業。』

19「那時他們人丁稀少,

寥寥可數,在當地寄居,

20他們在異國他鄉流離飄零。

21耶和華不容人壓迫他們,

還為他們的緣故責備君王,

22說,『不可加害我膏立的人,

也不可傷害我的先知。』

23「普世都要歌頌耶和華,

天天傳揚祂的救恩;

24要在列國述說祂的榮耀,

在萬民中述說祂的奇妙作為。

25因為耶和華無比偉大,

當受至高的頌揚;

祂超越一切神明,

當受敬畏。

26列邦的神明都是假的,

唯獨耶和華創造了諸天。

27祂帶著尊貴和威嚴,

祂的聖所充滿能力和喜樂。

28「萬族萬民啊,

要把榮耀和能力歸給耶和華,

歸給耶和華!

29要將耶和華之名當得的榮耀歸給祂,

要將供物獻給祂,

要穿聖衣敬拜耶和華16·29 或譯「要敬拜聖潔榮耀的耶和華」。

30大地要在祂面前顫抖;

世界堅立不搖。

31願天歡喜,願地快樂;

願他們在列國宣告,

『耶和華執掌王權!』

32願海洋和其中的萬物都歡呼,

願田野和其中的一切都歡騰!

33那時,林中的樹木都要在耶和華面前歡唱,

因為祂要來審判天下。

34你們要稱謝耶和華,

因為祂是美善的,

祂的慈愛永遠長存!

35「要說,『拯救我們的上帝啊,

求你拯救我們,招聚我們,

把我們從列國中救出來,

我們好稱謝你的聖名,

以讚美你為榮。』

36以色列的上帝耶和華永永遠遠當受稱頌!」

眾民都說:「阿們!」

並讚美耶和華。

分派事奉的人員

37大衛亞薩及其親族天天在約櫃前事奉耶和華,盡當盡的職分; 38又派俄別·以東及其六十八位親族、何薩耶杜頓的兒子俄別·以東守門; 39並派祭司撒督及其他祭司在基遍邱壇的耶和華的聖幕前供職, 40按照耶和華在律法書上對以色列人的吩咐,每日早晚在祭壇上獻燔祭給耶和華。 41與他們一同供職的有希幔耶杜頓和其他人,他們被特別選出來稱謝上帝,因為祂的慈愛永遠長存。 42希幔耶杜頓負責用號、鈸及其他樂器伴奏歌頌上帝。耶杜頓的子孫負責守門。 43於是,眾民各自回家,大衛也回去為家人祝福。