1 Nyakati 14 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version

1 Nyakati 14:1-17

Nyumba Ya Daudi Na Jamaa Yake

(2 Samweli 5:11-16)

114:1 1Fal 5:6; Hag 1:8; 2Sam 5:11Basi Hiramu mfalme wa Tiro akawatuma wajumbe kwa Daudi, wakiwa na magogo ya mierezi, waashi na maseremala ili kumjengea jumba la kifalme. 214:2 Hes 24:7; Kum 26:19Naye Daudi akatambua kwamba Bwana amemwimarisha kuwa mfalme juu ya Israeli na kwamba ufalme wake umetukuzwa kwa ajili ya Israeli, watu wake.

314:3 1Nya 3:1; Kum 17:14-17Huko Yerusalemu Daudi akaoa wake wengine zaidi na akawa baba wa wana na mabinti wengi. 414:4 2Sam 5:14; 1Nya 3:5Haya ndiyo majina ya watoto waliozaliwa kwake huko: Shamua, Shobabu, Nathani, Solomoni, 5Ibihari, Elishua, Elpeleti, 6Noga, Nefegi, Yafia, 7Elishama, Beeliada na Elifeleti.

Daudi Awashinda Wafilisti

(2 Samweli 5:17-25)

814:8 1Nya 11:1; 2Sam 5:17; Za 2:1-5Wafilisti waliposikia kuwa Daudi ametiwa mafuta kuwa mfalme wa Israeli yote, wakapanda na jeshi lao lote kwenda kumsaka, lakini Daudi akapata habari hizo, naye akatoka ili kwenda kukabiliana nao. 914:9 Yos 15:8; 1Nya 11:15Basi Wafilisti walikuwa wameingia na kushambulia Bonde la Warefai, 10Hivyo Daudi akamuuliza Mungu: “Je, niende kuwashambulia hao Wafilisti? Je, utawatia mikononi mwangu?”

Bwana akamjibu, “Nenda, nitawatia mikononi mwako.”

1114:11 Za 94:16; Isa 28:21Hivyo Daudi pamoja na watu wake wakakwea mpaka Baal-Perasimu,14:11 Maana yake ni Bwana Afurikae. akawashinda huko. Akasema, “Kama maji yafurikavyo, Mungu amewafurikia adui zangu kwa kutumia mkono wangu.” Kwa hiyo mahali pale pakaitwa Baal-Perasimu. 1214:12 Kut 32:20; Yos 7:15Wafilisti walikuwa wameacha miungu yao huko, Daudi akaamuru iteketezwe kwa moto.

1314:13 2Sam 5:22Kwa mara nyingine Wafilisti wakavamia lile bonde; 1414:14 Yos 8:6-7; 2Sam 5:23hivyo Daudi akamuuliza Mungu tena, naye Mungu akamjibu, “Usiwapandie moja kwa moja, bali wazungukie na uwashambulie kutoka mbele ya hiyo miti ya miforosadi. 15Mara usikiapo sauti ya kwenda juu ya hiyo miti ya miforosadi, hapo ndipo utoke upigane vita, kwa sababu hiyo itaonyesha kwamba Mungu amekutangulia ili kupiga jeshi la Wafilisti.” 1614:16 Yos 9:3; 10:33; 2Sam 5:25Kwa hiyo Daudi akafanya kama alivyoagizwa na Mungu, wakalipiga jeshi la Wafilisti kuanzia Gibeoni hadi Gezeri.

1714:17 Yos 6:27; 2Nya 26:8; Kum 2:25; Za 2:1-12Hivyo umaarufu wa Daudi ukaenea katika kila nchi, naye Bwana akayafanya mataifa yote kumwogopa Daudi.

Chinese Contemporary Bible 2023 (Traditional)

歷代志上 14:1-17

大衛的宮殿和家人

1泰爾希蘭差遣使者帶著香柏木、木匠和石匠去為大衛建造宮殿。 2那時,大衛知道耶和華已立他做以色列王,並因祂以色列子民的緣故而使他國家興旺。

3大衛耶路撒冷又娶了多位妻子,生了更多兒女。 4他在耶路撒冷生的孩子有沙姆亞朔罷拿單所羅門5益轄以利書亞以法列6挪迦尼斐雅非亞7以利沙瑪比利雅大以利法列

打敗非利士人

8非利士人聽說大衛已被膏立為以色列王,就全軍出動,搜尋大衛大衛聽說後,便出來迎敵。 9非利士人前來襲擊利乏音谷。 10大衛求問上帝:「我可以去迎戰非利士人嗎?你會把他們交在我手裡嗎?」耶和華說:「去吧,我必把他們交在你手裡。」

11於是,大衛前往巴力·毗拉心,在那裡打敗了他們。他說:「上帝藉我的手擊潰敵人,如洪水沖垮堤岸。」因此那地方叫巴力·毗拉心14·11 「巴力·毗拉心」意思是「沖垮之主」。12非利士人在那裡丟棄了他們的神像,大衛命人把它們燒掉。 13非利士人又來襲擊那山谷, 14大衛又求問上帝,上帝對他說:「你不要正面追擊他們,要繞到他們後面,從桑林對面攻打他們。 15你一聽見桑樹梢上響起腳步聲,就要進攻,因為那表示上帝已在你前頭去攻擊非利士的軍隊了。」 16大衛遵命而行,打敗非利士軍隊,從基遍一直殺到基色17於是,大衛名揚列國,耶和華使列國都懼怕他。