耶利米书 50 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

耶利米书 50:1-46

审判巴比伦的预言

1关于迦勒底人居住的巴比伦,耶和华对耶利米先知说:

2“你们要在列国中传扬和宣告,

要竖起旗帜,毫不隐瞒地宣告,

巴比伦要沦陷了!

她的神明彼勒必蒙羞,

米罗达必惊慌;

巴比伦的神像都蒙羞,

偶像都必惊慌。

3因为有一个来自北方的国家要攻击它,

使她的土地荒凉、人畜绝迹。’”

4耶和华说:“那时,以色列人要与犹大人一同来,流着泪寻求他们的上帝耶和华。 5他们必打听前往锡安的路,朝锡安走去。他们必凭永不被遗忘的约归附耶和华。 6我的子民成了一群迷路的羊,他们的牧人使他们步入歧途,在高山丘陵间流浪,忘了自己的安歇之处。 7遇见他们的人都吞噬他们。他们的敌人说,‘我们没有错!这是因为他们冒犯了他们真正的安歇之处——耶和华,他们祖先的盼望——耶和华。’ 8我的子民啊,你们要逃离巴比伦,离开迦勒底人的土地,要像带领羊群的公山羊一样离开。 9看啊,我要使来自北方的列强联合起来攻打巴比伦,他们要列阵攻占它,他们的勇士箭术高超,从不空手而归。 10他们要在迦勒底肆意掳掠,直到心满意足。这是耶和华说的。

11“抢夺我产业的巴比伦人啊,

你们欢喜快乐,

像草场上欢跳的母牛犊,

又像嘶鸣的公马。

12但你们的母亲巴比伦将羞愧难当,

生养你们的将蒙受耻辱,

她将排在列国之末,

沦为旷野、旱地和荒漠。

13由于耶和华的愤怒,

巴比伦必无人居住,

荒凉不堪。

她满目疮痍,

令路人惊惧、嗤笑。

14弓箭手啊,你们要列阵围攻巴比伦

向她猛射,

不要吝啬箭枝,

因为她得罪了耶和华。

15你们要从四面向她呐喊,

她必投降,

她的堡垒将倾倒,

城墙将坍塌,

因为耶和华要报应她。

你们要向她复仇,

她怎样对待别人,

你们也要怎样对待她。

16你们要铲除在巴比伦撒种的和收割的。

为躲避敌人的刀剑,

人们各自逃到故土亲族那里。

17以色列人是一群被狮子驱散的羊,先被亚述王吞噬,后被巴比伦尼布甲尼撒咬碎骨头。” 18因此,以色列的上帝——万军之耶和华说:“看啊,我要像惩罚亚述王一样惩罚巴比伦王和他的国家。 19我要带领以色列人返回他们的草场,让他们在迦密巴珊吃草,在以法莲基列的山上吃得饱足。 20那时,在以色列必找不到过犯,在犹大必找不到罪恶,因为我必赦免我保留下来的余民。这是耶和华说的。

21“你们要去攻打米拉大翁比割的居民,

照我的命令追杀他们,彻底消灭他们。

这是耶和华说的。

22巴比伦境内传来战争和大毁灭的声音。

23威震天下的锤子巴比伦竟被砍断、打碎了!

它的下场令列国震惊!

24巴比伦啊,我给你设下了陷阱,

你在懵然不知中被捉住,

你因为与耶和华为敌,

才被找到并擒获。

25耶和华已打开祂的兵器库,

取出倾泻祂烈怒的兵器。

因为主——万军之耶和华要惩罚迦勒底人。

26你们要从远方前来攻打巴比伦

打开她的粮仓,

使她沦为一堆废墟,

彻底毁灭她,不留一物。

27你们要杀掉她所有的士兵,

把他们全部屠杀。

他们大祸临头了,

惩罚他们的日子到了。

28“从巴比伦逃出来的人在锡安述说我们的上帝耶和华如何报仇,为祂的圣殿报仇。

29“要召集所有的弓箭手来攻打巴比伦,在她四围扎营,不让一人漏网。要照她的所作所为报应她;她怎样对待别人,也要怎样对待她,因为她藐视以色列的圣者耶和华。 30她的青年要倒毙街头,那时她所有的战士都要灭亡。”这是耶和华说的。

31“主——万军之耶和华说,

‘狂傲的人啊,我要与你为敌,

我惩罚你的时候到了。

32狂傲的人要踉踉跄跄,

跌倒在地,无人扶起。

我要焚烧她的城邑,

使她周围的一切化为灰烬。’”

33万军之耶和华说:“以色列人和犹大人要一同受压迫,掳走他们的人必控制他们,不肯释放他们。 34但他们的救赎主——万军之耶和华大有能力,祂必为他们申冤,使他们的家园安宁,使巴比伦的居民不得安宁。”

35耶和华说:

“敌人要攻击巴比伦的居民及其首领和谋士;

36敌人要攻击巴比伦的假先知,

使他们显出愚昧;

敌人要攻击巴比伦的勇士,

使他们充满恐惧;

37敌人要攻击巴比伦人的战车战马和他们的盟军,

使他们柔弱得像妇女;

敌人要攻打他们的库房,

肆意抢夺他们的财宝。

38旱灾必临到巴比伦

使那里的河流干涸,

因为那里神像遍地,

人们都沉迷于祭拜偶像。

39“因此,巴比伦必杳无人烟,永远荒凉,成为豺狼等野兽出没之地、鸵鸟的栖身之所。 40上帝要毁灭巴比伦,像毁灭所多玛蛾摩拉及其周围的城邑一样,使那里人烟绝迹。这是耶和华说的。

41“看啊,有一个民族要从北方来,

有一个强国及许多君王要从地极发动进攻。

42少女巴比伦啊,他们残酷无情,

手持弓箭和矛枪,

骑马奔来,声势如怒海狂涛,

列阵攻击你。

43巴比伦王听到风声,

四肢发软,痛苦不堪,

如分娩的妇人。

44“看啊,我必在瞬间把巴比伦人赶离家园,如约旦河边丛林中跳出的狮子赶散草场的羊群。我要派我拣选的人统治这地方。谁能与我相比?谁能与我较量?哪位首领能抵挡我?”

45因此,你们要听听耶和华攻击巴比伦的策略,听听祂攻击迦勒底人的计划。他们的孩子要被拖走,他们的家园要被毁灭。 46巴比伦被毁灭的消息震动大地,哭喊声传到列国。

Kiswahili Contemporary Version

Yeremia 50:1-46

Ujumbe Kuhusu Babeli

150:1 Isa 13:1; Za 137:8; Mwa 10:10Hili ndilo neno alilosema Bwana kupitia nabii Yeremia kuhusu Babeli na nchi ya Wakaldayo:

250:2 Kum 30:4; Yer 4:16; 51:31, 47; Isa 21:9; Za 20:5; Isa 13:2; Yer 46:6; Law 26:30“Tangazeni na mhubiri katikati ya mataifa,

twekeni bendera na mkahubiri;

msiache kitu chochote, bali semeni,

‘Babeli utatekwa;

Beli ataaibishwa,

Merodaki atajazwa na hofu kuu.

Sanamu zake zitaaibishwa

na vinyago vyake vitajazwa hofu kuu.’

350:3 Isa 14:22-23; Yer 9:11; Sef 1:3; Isa 13:17; 41:25; Yer 25:26Taifa kutoka kaskazini litamshambulia,

na kuifanya nchi yake ukiwa.

Hakuna hata mmoja atakayeishi ndani yake,

watu na wanyama wataikimbia.

450:4 Eze 37:22; Ezr 3:12; Yer 31:9; Isa 9:13; Hos 3:5; Yer 3:18“Katika siku hizo, wakati huo,”

asema Bwana,

“watu wa Israeli pamoja na watu wa Yuda

wataenda wakilia ili kumtafuta Bwana Mungu wao.

550:5 1Sam 29:1; Yer 33:7; Kum 29:14; Ebr 8:6-10; Isa 11:16; Yer 31:21; 32:40Wataiuliza njia iendayo Sayuni

na kuelekeza nyuso zao huko.

Watakuja na kuambatana na Bwana

katika agano la milele

ambalo halitasahaulika.

650:6 Isa 53:6; Mt 10:6; Yer 3:6; Eze 34:6; Za 119:176; Mt 9:36; Yer 10:21; Za 95:10“Watu wangu wamekuwa kondoo waliopotea;

wachungaji wao wamewapotosha

na kuwasababisha kuzurura

juu ya milima.

Walitangatanga juu ya mlima na kilima,

na kusahau mahali pao wenyewe pa kupumzikia.

750:7 Yer 2:3; 14:8; Za 22:4; Yer 5:17; 10:25; Eze 35:12Yeyote aliyewakuta aliwala;

adui zao walisema, ‘Sisi hatuna hatia,

kwa kuwa wao walitenda dhambi dhidi ya Bwana, malisho yao halisi,

Bwana, aliye tumaini la baba zao.’

850:8 Isa 48:20; Ufu 18:4; Yer 51:6“Kimbieni kutoka Babeli;

ondokeni katika nchi ya Wakaldayo

tena kuweni kama mbuzi wale waongozao kundi.

950:9 Isa 13:17; Yer 25:14; Isa 41:25; Yer 25:26Kwa maana nitaamsha na kuleta dhidi ya Babeli

muungano wa mataifa makubwa kutoka nchi ya kaskazini.

Watashika nafasi zao dhidi yake,

naye kutokea kaskazini atatekwa.

Mishale yao itakuwa kama mishale ya mashujaa walio hodari,

ambao hawawezi kurudi mikono mitupu.

10Kwa hiyo Ukaldayo utatekwa nyara;

wote wamtekao nyara watapata za kutosha,”

asema Bwana.

1150:11 Isa 47:6; Yer 31:18“Kwa sababu hushangilia na kufurahi,

wewe utekaye urithi wangu,

kwa sababu unachezacheza kama mtamba anayepura nafaka,

na kulia kama farasi dume,

1250:12 Yer 51:47; 25:12; 51:26mama yako ataaibika mno,

yeye aliyekuzaa atatahayari.

Atakuwa mdogo kuliko mataifa mengine yote,

atakuwa nyika, nchi kame na jangwa.

1350:13 Eze 27:36; Hab 2:6; Kum 29:22; Yer 49:17; 9:11; 48:9; 51:62; 18:16Kwa sababu ya hasira ya Bwana hatakaliwa na mtu,

lakini ataachwa ukiwa kabisa.

Wote watakaopita Babeli watatiwa hofu na kudhihaki

kwa sababu ya majeraha yake yote.

14“Shikeni nafasi zenu kuzunguka Babeli,

enyi nyote mvutao upinde.

Mpigeni! Msibakize mshale wowote,

kwa kuwa ametenda dhambi dhidi ya Bwana.

1550:15 Yer 51:14; 2Nya 30:8; Yer 51:44-58; 2Fal 25:4; Yer 51:6; Ufu 18:6; Isa 10:3; Hab 2:7-8Piga kelele dhidi yake kila upande!

Anajisalimisha, minara yake inaanguka,

kuta zake zimebomoka.

Kwa kuwa hiki ni kisasi cha Bwana,

mlipizeni kisasi;

mtendeeni kama alivyowatendea wengine.

1650:16 Yer 25:38; Isa 13:14; Yer 51:9Katilieni mbali mpanzi kutoka Babeli,

pamoja na mvunaji na mundu wake akivuna.

Kwa sababu ya upanga wa mdhalimu

kila mmoja na arejee kwa watu wake mwenyewe,

kila mmoja na akimbilie

kwenye nchi yake mwenyewe.

1750:17 2Fal 24:1; Yer 2:15; Kum 4:27; 2Fal 17:6; 24:10-17; 1Pet 2:25; Yer 2:15; Hes 24:8“Israeli ni kundi lililotawanyika

ambalo simba wamelifukuzia mbali.

Wa kwanza kumla alikuwa mfalme wa Ashuru,

wa mwisho kuponda mifupa yake

alikuwa Nebukadneza mfalme wa Babeli.”

1850:18 Isa 10:12; Eze 31:3; Sef 2:13Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo:

“Nitamwadhibu mfalme wa Babeli na nchi yake

kama nilivyomwadhibu mfalme wa Ashuru.

1950:19 Yer 31:10; Eze 34:13; Yer 33:12; Isa 65:10; Mik 7:14; Zek 10:10Lakini nitamrudisha Israeli katika malisho yake mwenyewe

naye atalisha huko Karmeli na Bashani;

njaa yake itashibishwa

juu ya vilima vya Efraimu na Gileadi.

2050:20 Za 103:12; Zek 3:4-9; Isa 33:24; Yer 31:34; Rum 9:27; Isa 10:20-22; Eze 36:16Katika siku hizo, wakati huo,”

asema Bwana,

“uchunguzi utafanyika kwa ajili ya kosa la Israeli,

lakini halitakuwepo,

kwa ajili ya dhambi za Yuda,

lakini haitapatikana hata moja,

kwa kuwa nitawasamehe

mabaki nitakaowaacha.

2150:21 Eze 23:23; Isa 10:6“Shambulieni nchi ya Merathaimu

na wale waishio huko Pekodi.

Wafuatieni, waueni

na kuwaangamiza kabisa,”

asema Bwana.

“Fanyeni kila kitu nilichowaamuru.

2250:22 Yer 4:19-21; 51:54Kelele ya vita iko ndani ya nchi,

kelele ya maangamizi makuu!

2350:23 Isa 14:16; Yer 51:20; Isa 10:5Tazama jinsi nyundo ya dunia yote

ilivyovunjika na kuharibika!

Tazama jinsi Babeli ilivyokuwa ukiwa

miongoni mwa mataifa!

2450:24 Yer 51:12; Dan 5:30-31; Yer 51:31; Ay 9:4Nimetega mtego kwa ajili yako, ee Babeli,

nawe ukakamatwa kabla haujafahamu;

ulipatikana na ukakamatwa

kwa sababu ulimpinga Bwana.

2550:25 Isa 13:5Bwana amefungua ghala lake la silaha

na kuzitoa silaha za ghadhabu yake,

kwa kuwa Bwana Mwenyezi Mwenye Nguvu Zote

anayo kazi ya kufanya

katika nchi ya Wakaldayo.

2650:26 Isa 14:22-23; Yer 51:11; Rut 3:7Njooni dhidi yake kutoka mbali.

Zifungueni ghala zake za nafaka;

mlundikeni kama lundo la nafaka.

Mwangamizeni kabisa

na msimwachie mabaki yoyote.

2750:27 Za 68:30; Yer 48:15; Ay 18:20; Yer 25:34Waueni mafahali wake wachanga wote;

waacheni washuke machinjoni!

Ole wao! Kwa kuwa siku yao imewadia,

wakati wao wa kuadhibiwa.

2850:28 Isa 48:20; Yer 51:10; 2Fal 24:13; Yer 52:13Wasikilizeni watoro na wakimbizi kutoka Babeli

wakitangaza katika Sayuni

jinsi Bwana, Mungu wetu alivyolipiza kisasi,

kisasi kwa ajili ya Hekalu lake.

2950:29 Ay 21:19; Ufu 18:6; Oba 1:15; Dan 5:23; Isa 14:13-14; Mao 3:24; Isa 13:18; Kum 32:41“Waiteni wapiga mishale dhidi ya Babeli,

wote wale wavutao upinde.

Pigeni kambi kumzunguka kabisa,

asitoroke mtu yeyote.

Mlipizeni kwa matendo yake;

mtendeeni kama alivyotenda.

Kwa kuwa alimdharau Bwana,

yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.

3050:30 Isa 13:18; Yer 49:26; 51:4Kwa hiyo, vijana wake wanaume wataanguka barabarani;

askari wake wote watanyamazishwa siku ile,”

asema Bwana.

3150:31 Yer 21:13; Ufu 18:7-8“Tazama, niko kinyume nawe, ewe mwenye majivuno,”

asema Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote,

“kwa kuwa siku yako imewadia,

yaani, wakati wako wa kuadhibiwa.

3250:32 Yer 21:14; 49:27; Amo 5:2; Za 20:8; 119:21Mwenye majivuno atajikwaa na kuanguka,

wala hakuna yeyote atakayemuinua;

nitawasha moto katika miji yake,

utakaowateketeza wote wanaomzunguka.”

3350:33 Isa 58:6; 14:17Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote:

“Watu wa Israeli wameonewa,

nao watu wa Yuda pia.

Wote waliowateka wamewashikilia sana,

wanakataa kuwaachia waende.

3450:34 Yer 31:35; 51:19; Za 119:154; Mao 3:58; Kut 6:6; Ay 19:25; Isa 49:25Lakini Mkombozi wao ana nguvu;

Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake.

Atatetea kwa nguvu shauri lao

ili alete raha katika nchi yao,

lakini ataleta msukosuko

kwa wale waishio Babeli.

3550:35 Yer 47:6; Dan 5:7; Isa 37:13; 45:1“Upanga dhidi ya Wakaldayo!”

asema Bwana,

“dhidi ya wale waishio Babeli

na dhidi ya maafisa wake na watu wenye busara!

36Upanga dhidi ya manabii wake wa uongo!

Watakuwa wapumbavu.

Upanga dhidi ya mashujaa wake!

Watajazwa na hofu kuu

3750:37 Yer 25:20; 2Fal 19:23; Isa 19:16; Yer 51:21; Nah 3:13; Isa 45:3Upanga dhidi ya farasi na magari yake ya vita

pamoja na askari wake wote wa kigeni katika safu zake!

Wao watakuwa kama wanawake.

Upanga dhidi ya hazina zake!

Hizo zitatekwa nyara.

3850:38 Isa 11:15; Yer 51:36; Ufu 16:12Ukame juu ya maji yake!

Nayo yatakauka.

Kwa kuwa ni nchi ya sanamu,

wao wanaenda wazimu kwa ajili ya sanamu.

3950:39 Isa 34:13-15; Ufu 18:2; Isa 13:19-22; Za 74:14; Yer 51:37“Kwa hiyo, viumbe vya jangwani na fisi wataishi humo,

nao bundi watakaa humo.

Kamwe haitakaliwa tena

wala watu hawataishi humo kutoka kizazi hadi kizazi.

4050:40 Mwa 19:24; Mt 10:15; 2Pet 2:6; Yer 51:62Kama vile Mungu alivyoangamiza Sodoma na Gomora

pamoja na miji iliyokuwa jirani nayo,”

asema Bwana,

“vivyo hivyo hakuna mtu yeyote

atakayeishi humo.

Naam, hakuna mtu yeyote

atakayekaa humo.

4150:41 Isa 41:25; Yer 6:22; Isa 13:14; Yer 51:22-28; Ufu 17:16; Isa 23:17“Tazama! Jeshi linakuja kutoka kaskazini;

taifa kubwa na wafalme wengi

wanaamshwa kutoka miisho ya dunia.

4250:42 Isa 13:18; 5:30; 47:1; Yer 6:23; Ay 30:21Wamejifunga pinde na mikuki;

ni wakatili na wasio na huruma.

Wanatoa sauti kama bahari inayonguruma

wanapoendesha farasi zao;

wanakuja kama watu waliojipanga tayari kwa vita

ili kukushambulia, ee Binti Babeli.

4350:43 Yer 47:3; 6:22-24Mfalme wa Babeli amesikia habari kuwahusu,

nayo mikono yake imelegea.

Uchungu umemshika,

maumivu kama ya mwanamke katika utungu wa kuzaa.

4450:44 Hes 16:5; Ay 41:10; Isa 46:9; Yer 12:5; 49:19Kama simba anayepanda kutoka vichaka vya Yordani

kuja kwenye nchi ya malisho mengi,

ndivyo nitamfukuza Babeli kutoka nchi yake ghafula.

Ni nani aliye mteule,

nitakayemweka kwa ajili ya jambo hili?

Ni nani aliye kama mimi,

na ni nani awezaye kunipinga?

Tena ni mchungaji yupi

awezaye kusimama kinyume nami?”

4550:45 Isa 24:14; Mdo 4:28; Isa 48:14; Yer 51:11Kwa hiyo, sikia kile Bwana alichokipanga dhidi ya Babeli,

kile alichokusudia dhidi ya nchi ya Wakaldayo:

Aliye mchanga katika kundi ataburutwa mbali.

Yeye ataharibu kabisa malisho yao kwa sababu yao.

4650:46 Ay 24:12; Ufu 18:9-10; Amu 5:4; Yer 49:21Kwa sauti ya kutekwa kwa Babeli, dunia itatetemeka;

kilio chake kitasikika pote miongoni mwa mataifa.