以赛亚书 41 – CCB & NEN

Chinese Contemporary Bible 2022 (Simplified)

以赛亚书 41:1-29

上帝是以色列的帮助

1上帝说:“众海岛啊,

要在我面前安静!

让众民重新得力,

让他们前来说话,

让我们一起来理论。

2“谁使一人从东方兴起?

谁凭公义把他召到跟前?

谁把列国交给他,

使他征服列国的君王,

用刀将他们化为尘土,

用弓驱散他们如风吹的碎秸?

3他追赶他们,

安然走过从未踏足之路。

4谁成就了这事?

谁从太初就决定各个世代?

是我耶和华,

我太初就在那里,

末了也在那里。

5“众海岛看见就害怕,

地极也颤抖,

他们都上前来,

6彼此帮助,

互相勉励说,‘要刚强!’

7工匠鼓励金匠,

打磨的勉励打砧的,

谈到焊接的说,‘焊得好!’

他们用钉子把偶像钉牢,免得摇晃。

8“然而,以色列啊,你是我的仆人;

雅各啊,你是我拣选的,

是我朋友亚伯拉罕的后裔。

9我把你从地极带来,

从遥远的角落召来。

我对你说,‘你是我的仆人,

我拣选了你,没有丢弃你。

10你不要害怕,因为我与你同在,

你不要惊慌,因为我是你的上帝。

我必赐你力量,帮助你,

用我公义的右手扶持你。’

11“看啊,凡向你发怒的人必抱愧蒙羞;

与你为敌的人都要灭亡,

归于无有。

12你寻找与你相争的人,

却找不到;

与你争战的人必归于无有。

13因为我是你的上帝耶和华,

我拉着你的右手对你说,

‘不要怕,我必帮助你。’

14“蠕虫雅各啊,以色列人啊,不要怕!

你的救赎主——以色列的圣者耶和华说,

‘我必帮助你。’

15看啊,我要使你成为一具簇新、

带许多利齿的打谷器。

你要打碎高山,

使丘陵碎如糠秕。

16你要簸它们,让风吹散它们,

让狂风卷走它们。

但你要以耶和华为喜乐,

以色列的圣者为荣耀。

17“贫穷困苦的人找不到水喝,

他们口干舌燥。

但我耶和华必应允他们的呼求,

我,以色列的上帝不会撇弃他们。

18我要使光秃的山岭上江河奔流,

山谷中泉水涌流;

我要使沙漠变成水塘,

使干地冒出泉水。

19我要在旷野栽种香柏树、

皂荚树、番石榴树和橄榄树。

我要在沙漠种松树、杉树和黄杨树,

20好让人一看就知道,

一想就明白,

这是耶和华亲手所为,

以色列的圣者创造的。”

21耶和华对偶像说:

“陈明你们的主张吧。”

雅各的王说:

“摆出你们的证据吧。”

22告诉我们将要发生的事,

告诉我们以前发生的事,

我们好思想并明白事情的结局。

向我们宣告将来的事,

23告诉我们以后会发生什么,

好叫我们知道你们是神明。

不论降福降祸,

好叫我们一同惊惧!

24看啊,你们实在算不得什么,

你们所做的毫无意义,

选择你们的人真是可憎!

25“我使一人从北方兴起,

他来了,

他在东方求告我的名。

他必把掌权者像灰泥一样踏在脚下,

像窑匠踩泥一样。

26谁从太初就宣告这事,让我们知道呢?

谁预先讲明这事,让我们说他是对的呢?

谁也没有宣告过,

谁也没有预言过,

谁也没有听见你们说什么。

27是我首先告诉锡安的,

我给耶路撒冷一个报好消息的使者。

28我看了看,没有一个出谋划策的。

我问话,没有一个回答。

29看啊,偶像全是假的,

毫无作为,铸像虚空如风。

Kiswahili Contemporary Version

Isaya 41:1-29

Msaidizi Wa Israeli

141:1 Za 37:7; Isa 48:16; 50:8; Hab 2:20; Zek 2:13; Isa 11:11; 1Sam 2:4“Nyamazeni kimya mbele zangu, enyi visiwa!

Mataifa na wafanye upya nguvu zao!

Wao na wajitokeze, kisha waseme,

tukutane pamoja mahali pa hukumu.

241:2 2Sam 22:43; Isa 40:24; Yer 51:11; Ezr 1:2; Isa 44:28; Yer 50:3; 25:9“Ni nani aliyemchochea mmoja kutoka mashariki,

akimwita katika haki kwa utumishi wake?

Huyatia mataifa mikononi mwake,

na kuwatiisha wafalme mbele zake.

Huwafanya kuwa mavumbi kwa upanga wake,

huwafanya makapi yapeperushwayo na upepo kwa upinde wake.

341:3 Dan 8:4Huwafuatia na kuendelea salama,

katika njia ambayo miguu yake haijawahi kupita.

441:4 Isa 48:12; Ufu 22:13; Mdo 15:18; Isa 43:7; Kum 32:29Ni nani aliyefanya jambo hili na kulitimiliza,

akiita vizazi tangu mwanzo?

Mimi, Bwana, ni wa kwanza

nami nitakuwa pamoja na wa mwisho:

mimi Bwana ndiye.”

541:5 Eze 26:17-18; Kum 30:4; Isa 11:11-12Visiwa vimeliona na kuogopa,

miisho ya dunia inatetemeka.

Wanakaribia na kuja mbele,

641:6 Isa 1:6kila mmoja humsaidia mwingine

na kusema kwa ndugu yake, “Uwe hodari!”

741:7 Isa 40:19; 44:13; Yer 30:3-5Fundi humtia moyo sonara,

yeye alainishaye kwa nyundo

humhimiza yeye agongeaye kwenye fuawe,

Humwambia yeye aunganishaye, “Ni kazi njema.”

Naye huikaza sanamu kwa misumari ili isitikisike.

841:8 Mwa 18:19; Isa 29:22; Neh 9:7; 2Nya 20:7; Yak 2:23; Isa 63:16; Za 136:22“Lakini wewe, ee Israeli, mtumishi wangu,

Yakobo, niliyemchagua,

ninyi wazao wa Abrahamu rafiki yangu,

941:9 Isa 37:16; Kum 7:6; Isa 20:3; 11:12nilikuchukua toka miisho ya dunia,

nilikuita kutoka pembe zake za mbali.

Nilisema, ‘Wewe ni mtumishi wangu’;

nimekuchagua, wala sikukukataa.

1041:10 Kum 3:22; Rum 8:3; Isa 49:8; Yer 30:10; 46:27-28; Ay 40:14; Za 18:35Hivyo usiogope, kwa maana niko pamoja nawe;

usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako.

Nitakutia nguvu na kukusaidia;

nitakutegemeza kwa mkono wa kuume wa haki yangu.

1141:11 Isa 17:12; 54:17; Kut 23:22; Isa 29:8; Zek 12:3; Yer 2:3; Isa 29:23“Wote walioona hasira dhidi yako

hakika wataaibika na kutahayarika,

wale wakupingao

watakuwa kama vile si kitu, na kuangamia.

1241:12 Za 37:35-36; Isa 34:12; Ay 7:8; Isa 29:20; 17:14Ingawa utawatafuta adui zako,

hutawaona.

Wale wanaopigana vita dhidi yako

watakuwa kama vile si kitu kabisa.

1341:13 Za 73:23; Isa 42:6; 45:1; 51:18Kwa maana Mimi ndimi Bwana, Mungu wako,

nikushikaye mkono wako wa kuume

na kukuambia, Usiwe na hofu,

nitakusaidia.

1441:14 Ay 4:19; Za 22:6; Kut 15:13; Ay 19:23; Isa 1:27Usiogope, ee Yakobo uliye mdudu,

ee Israeli uliye mdogo,

kwa kuwa Mimi mwenyewe nitakusaidia,” asema Bwana,

Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.

1541:15 Ay 41:30; Mik 4:13; Isa 21:10; Kut 19:18; Yer 9:10; Eze 33:28“Tazama, nitakufanya chombo cha kupuria,

kipya na chenye makali, chenye meno mengi.

Utaipura milima na kuiponda

na kuvifanya vilima kuwa kama makapi.

1641:16 Yer 51:2; Isa 45:25; 60:19; Dan 2:35; Yer 15:7; Isa 25:9; Mk 1:24Utaipepeta, nao upepo utaichukua,

dhoruba itaipeperushia mbali.

Bali wewe utajifurahisha katika Bwana

na katika utukufu wa yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.

1741:17 Isa 43:20; 35:7; 30:19“Maskini na wahitaji wanatafuta maji,

lakini hayapo,

ndimi zao zimekauka kwa kiu.

Lakini Mimi Bwana nitawajibu,

Mimi, Mungu wa Israeli, sitawaacha.

1841:18 Isa 30:25; 43:19; Ay 38:26; Isa 35:7; 2Fal 3:17Nitaifanya mito itiririke juu ya vilima vilivyo kame,

nazo chemchemi ndani ya mabonde.

Nitaligeuza jangwa liwe mabwawa ya maji,

nayo ardhi iliyokauka kuwa chemchemi za maji.

1941:19 Isa 60:13; Kut 25:10-13; Isa 37:24; 44:14Katika jangwa nitaotesha

mwerezi, mshita, mhadasi na mzeituni.

Nitaweka misunobari, mivinje na misanduku

pamoja huko nyikani,

2041:20 Ay 12:9; Isa 4:5ili kwamba watu wapate kuona na kujua,

wapate kufikiri na kuelewa,

kwamba mkono wa Bwana umetenda hili,

kwamba yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli ndiye alilifanya.”

2141:21 Isa 43:14; 44:6Bwana asema, “Leta shauri lako.

Toa hoja yako,” asema Mfalme wa Yakobo.

2241:22 Isa 48:14; 65:17; Yn 13:19; Isa 43:9; 45:21“Leteni sanamu zenu zituambie

ni nini kitakachotokea.

Tuambieni mambo ya zamani yalikuwa nini,

ili tupate kuyatafakari

na kujua matokeo yake ya mwisho.

Au tutangazieni mambo yatakayokuja,

2341:23 Kum 18:22; Isa 44:7-8; Yer 10:5; Isa 43:5; 2Fal 19:26tuambieni ni nini kitakachotokea baadaye,

ili tupate kujua kuwa ninyi ni miungu.

Fanyeni jambo lolote zuri au baya,

ili tupate kutishika na kujazwa na hofu.

2441:24 Isa 37:19; 1Kor 8:4; Za 115:8; 1Sam 12:21; Isa 48:8Lakini ninyi ni zaidi ya bure kabisa,

na kazi zenu hazifai kitu kabisa;

yeye awachaguaye ni chukizo sana.

2541:25 Yer 51:48; Nah 3:14; 2Sam 22:43; Yer 50:9“Nimemchochea mtu mmoja kutoka kaskazini,

naye yuaja, mmoja toka mawio ya jua aliitaye Jina langu.

Huwakanyaga watawala kana kwamba ni matope,

kama mfinyanzi akanyagavyo udongo wa kufinyangia.

2641:26 Hab 2:18-19; 1Fal 18:26; Isa 52:6Ni nani aliyenena hili tokea mwanzoni, ili tupate kujua,

au kabla, ili tuweze kusema, ‘Alikuwa sawa’?

Hakuna aliyenena hili,

hakuna aliyetangulia kusema hili,

hakuna yeyote aliyesikia maneno kutoka kwenu.

2741:27 Isa 48:3, 16; 40:9Nilikuwa wa kwanza kumwambia Sayuni,

‘Tazama, wako hapa!’

Nilimpa Yerusalemu mjumbe wa habari njema.

2841:28 Eze 22:30; Za 22:11; Isa 40:13-14; 50:2; 59:16; 64:7; Yer 25:4Ninatazama, lakini hakuna yeyote:

hakuna yeyote miongoni mwao awezaye kutoa shauri,

hakuna yeyote wa kutoa jibu wakati ninapowauliza.

2941:29 Yer 5:13; 1Sam 12:21; Isa 37:19Tazama, wote ni ubatili!

Matendo yao ni bure;

vinyago vyao ni upepo mtupu na machafuko.