Zaburi 71:9-18
71:9 Za 51:11; 92:14; Kum 4:31; 31:6Usinitupe wakati wa uzee,
wala usiniache nguvu zangu zinapopungua.
71:10 Za 3:7; 10:8; 59:3; 31:13; Mt 1:10; 12:14Kwa maana adui zangu wananisengenya,
wale wanaonivizia kuniua wafanya hila.
71:11 Isa 40:27; 54:7; Mt 27:46; Za 7:2; 9:10; Mao 5:20Wanasema, “Mungu amemwacha,
mkimbilieni mkamkamate,
kwani hakuna wa kumwokoa.”
71:12 Za 38:21, 22; 22:19Ee Mungu, usiwe mbali nami,
njoo haraka kunisaidia, Ee Mungu wangu.
71:13 Ay 8:22; Za 15:3; 70:2; Yer 18:19Washtaki wangu na waangamie kwa aibu,
wale wanaotaka kunidhuru
na wafunikwe kwa dharau na fedheha.
71:14 Za 25:3; 42:5; 130:7; 131:3Lakini mimi, nitatumaini siku zote,
nitakusifu zaidi na zaidi.
71:15 Za 71:8; 66:6; 51:14Kinywa changu kitasimulia haki yako,
wokovu wako mchana kutwa,
ingawa sifahamu kipimo chake.
71:16 Za 77:12; 106:2; 118:15; 9:1; 145:4Ee Bwana Mwenyezi, nitakuja
na kutangaza matendo yako makuu,
nitatangaza haki yako, yako peke yako.
71:17 Yer 7:13; Ay 5:9; Za 26:7; 86:10; 96:3; Kum 4:5Ee Mungu, umenifundisha tangu ujana wangu,
hadi leo ninatangaza matendo yako ya ajabu.
71:18 Isa 46:4; Kut 9:16; Ay 8:8; Yoe 1:3; Za 78:4; 145:4; 22:30, 31Ee Mungu, usiniache,
hata niwapo mzee wa mvi,
mpaka nitangaze uwezo wako kwa kizazi kijacho,
nguvu zako kwa wote watakaokuja baadaye.