Zaburi 60:5-12
60:5 Ay 40:14; Kum 33:12; Za 108:6Tuokoe na utusaidie kwa mkono wako wa kuume,
ili wale uwapendao wapate kuokolewa.
60:6 Mwa 12:6; 33:17; Za 89:35; Yos 13:27Mungu amenena kutoka patakatifu pake:
“Nitaigawa Shekemu kwa ushindi
na kulipima Bonde la Sukothi.
60:7 Yos 13:31; Hes 34:19; Mwa 41:52; 49:10; Kum 33:17Gileadi ni yangu na Manase ni yangu;
Efraimu ni kofia yangu ya chuma,
nayo Yuda ni fimbo yangu ya utawala.
60:8 2Sam 8:1Moabu ni sinia langu la kunawia,
juu ya Edomu natupa kiatu changu;
nashangilia kwa kushindwa kwa Ufilisti.”
Ni nani atakayenipeleka hadi mji wenye ngome?
Ni nani atakayeniongoza hadi nifike Edomu?
60:10 Yos 7:12; Za 44:9Ee Mungu, si ni wewe uliyetukataa sisi,
na hutoki tena na majeshi yetu?
60:11 Za 146:3; Mit 3:5Tuletee msaada dhidi ya adui,
kwa maana msaada wa mwanadamu haufai kitu.
60:12 1Nya 19:13; Ay 40:12; Za 44:5Kwa msaada wa Mungu tutapata ushindi,
naye atawaponda adui zetu.