Zaburi 22:22-31
22:22 Za 26:12; 35:18; 40:9, 10; 68:26; Ebr 2:12; Yn 20:17Nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu,
katika kusanyiko nitakusifu wewe.
22:23 Yer 3:17; Za 66:8; 33:2, 8; 103:1; 86:12; 106:1; 50:15; 113:1; 117:1; 135:19; Isa 24:15; 25:3; 49:23; 60:9; Kum 14:23Ninyi ambao mnamcha Bwana, msifuni!
Ninyi nyote wazao wote wa Yakobo, mheshimuni yeye!
Mcheni yeye, ninyi wazao wote wa Israeli!
22:24 Ebr 5:7; Za 9:12; 102:17; 13:1; 27:9; 69:17; 102:2; 143:7; Ay 24:12; 36:5Kwa maana hakupuuza wala kudharau
mateso ya aliyeonewa;
hakumficha uso wake
bali alisikiliza kilio chake ili amsaidie.
22:25 Za 26:12; 35:18; 40:9; 82:1; Hes 30:2Kwako wewe hutoka kiini cha sifa zangu katika kusanyiko kubwa,
nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wakuchao wewe.
22:26 Za 107:9; 40:16Maskini watakula na kushiba,
wale wamtafutao Bwana watamsifu:
mioyo yenu na iishi milele!
22:27 Za 2:8; 86:9; 102:22; Dan 7:27; Mik 4:1Miisho yote ya dunia itakumbuka
na kumgeukia Bwana,
nazo jamaa zote za mataifa
watasujudu mbele zake,
22:28 Za 47:7; Zek 14:9; Mt 6:13kwa maana ufalme ni wa Bwana
naye hutawala juu ya mataifa.
22:29 Za 45:12; 89:48; 95:6; 96:9; 99:5; Isa 26:19; 27:13; 49:7; 66:23; Zek 14:16Matajiri wote wa dunia watasherehekea na kuabudu.
Wote waendao mavumbini
watapiga magoti mbele yake,
wote ambao hawawezi
kudumisha uhai wao.
22:30 Isa 53:10; 54:3; 61:9; 66:22; Za 102:18Wazao wa baadaye watamtumikia yeye;
vizazi vijavyo vitajulishwa habari za Bwana.
22:31 Za 5:8; 71:18; 78:6; 40:9; 102:18; Lk 18:31; 24:44Watatangaza haki yake kwa watu
ambao hawajazaliwa bado,
kwa maana yeye ametenda hili.