Zaburi 119:169-176
Kuomba Msaada
119:169 Ay 16:18; Za 119:9, 34Ee Bwana, kilio changu na kifike mbele zako,
nipe ufahamu sawasawa na neno lako.
119:170 1Fal 8:30; 2Nya 6:24; Za 28:2; 140:6; 143:1; 3:7; 22:20; 59:1; 119:41Maombi yangu na yafike mbele zako,
niokoe sawasawa na ahadi yako.
119:171 Za 51:15; 63:3; 94:12; Isa 2:3; Mik 4:2Midomo yangu na ibubujike sifa,
kwa kuwa unanifundisha maagizo yako.
119:172 Za 51:14; 119:7, 75Ulimi wangu na uimbe kuhusu neno lako,
kwa kuwa amri zako zote ni za haki.
119:173 Za 37:24; 73:23; Isa 41:10; Lk 10:42; Yos 24:22; Mit 1:29Mkono wako uwe tayari kunisaidia,
kwa kuwa nimechagua mausia yako.
119:174 Za 119:16, 24, 166Ee Bwana, ninatamani wokovu wako,
na sheria yako ni furaha yangu.
119:175 Za 119:116, 159; Isa 55:3Nijalie kuishi ili nipate kukusifu,
na sheria zako zinitegemeze.
119:176 Za 119:10; 95:10; Yer 50:17; Eze 34:11; Lk 15:4Nimetangatanga kama kondoo aliyepotea.
Mtafute mtumishi wako,
kwa kuwa sijasahau amri zako.