Zaburi 115:12-18
115:12 1Nya 16:15; Mwa 12:2; Efe 1:3Bwana anatukumbuka na atatubariki:
ataibariki nyumba ya Israeli,
ataibariki nyumba ya Aroni,
115:13 Za 24:4; 112:1; Law 26:3; Mit 10:6; Kum 11:27atawabariki wale wanaomcha Bwana,
wadogo kwa wakubwa.
115:14 Kum 1:11Bwana na awawezeshe kuongezeka,
ninyi na watoto wenu.
115:15 Mdo 14:15; Ufu 10:6; Za 96:5; Mwa 1:1; 14:19Mbarikiwe na Bwana
Muumba wa mbingu na dunia.
115:16 Za 89:11; Mwa 1:28; 8:6-8Mbingu zilizo juu sana ni mali ya Bwana,
lakini dunia amempa mwanadamu.
115:17 Za 88:10-12Sio wafu wanaomsifu Bwana,
wale washukao mahali pa kimya,115:17 Mahali pa kimya maana yake ni Kuzimu, yaani Sheol kwa Kiebrania.
115:18 Za 111:1; 113:2; 28:6; 33:2; 105:1; 145:2; Dan 2:20bali ni sisi tunaomtukuza Bwana,
sasa na hata milele.
Msifuni Bwana.115:18 Msifuni Bwana ni Kiebrania Hallelu Yah.