Mithali 2:12-22
2:12 Mit 2:16; 3:13-18; 4:5Hekima itakuokoa kutoka njia za waovu,
kutoka kwa watu ambao maneno yao yamepotoka,
2:13 Mit 4:19; Yn 3:19; Efe 4:18wale waachao mapito yaliyonyooka
wakatembea katika njia za giza,
2:14 Mit 15:21; Yer 11:15wale wapendao kutenda mabaya
na kufurahia upotovu wa ubaya,
2:15 Za 125:5; Mit 21:8ambao mapito yao yamepotoka
na ambao ni wapotovu katika njia zao.
2:16 Mit 6:20-29; 7:5-27Itakuokoa pia kutokana na mwanamke kahaba,
kutokana na mke aliyepotoka mwenye maneno
ya kushawishi kutenda ubaya,
2:17 Mal 2:14; Mwa 2:24aliyemwacha mwenzi wa ujana wake
na kupuuza agano alilofanya mbele ya Mungu.
2:18 Mit 5:5; 7:27; 9:18Kwa maana nyumba yake huelekea kwenye kifo
na mapito yake kwenye roho za waliokufa.
2:19 Mit 5:8; Mhu 7:26; Ebr 13:4Hakuna yeyote aendaye kwake akarudi,
au kufikia mapito ya uzima.
2:20 Ebr 6:12Hivyo utatembea katika njia za watu wema
na kushikamana na mapito ya wenye haki.
2:21 Za 37:29Kwa maana wanyofu wataishi katika nchi,
nao wasio na lawama watabakia ndani yake.
2:22 Ay 18:17; Za 37:38; Kum 29:28Bali waovu watakatiliwa mbali kutoka nchi,
nao wasio waaminifu watangʼolewa kutoka humo.