Ayubu 19:1-29, Ayubu 20:1-29, Ayubu 21:1-34 NEN

Ayubu 19:1-29

Hotuba Ya Sita Ya Ayubu

Ayubu Anajibu: Najua Mkombozi Wangu Yu Hai

Ndipo Ayubu akajibu:

19:2 1Sam 1:6; Za 6:2, 3; Ay 6:9; 13:25“Je, mtaendelea kunitesa mpaka lini,

na kuniponda kwa maneno yenu?

19:3 Mwa 31:7; Ay 20:3Mara kumi hizi mmenishutumu;

bila aibu mnanishambulia.

19:4 Ay 6:24; Za 19:12; Eze 18:4Kama ni kweli nimepotoka,

kosa langu ninabaki kuhusika nalo mwenyewe.

19:5 Za 38:16; 55:12; Mik 7:8Kama kweli mngejitukuza wenyewe juu yangu,

na kutumia unyonge wangu dhidi yangu,

19:6 Ay 6:29; 18:8; 10:3basi jueni kuwa Mungu amenitendea yaliyo mabaya,

naye amekokota wavu wake kunizunguka.

19:7 Ay 9:24; 30:20; Za 22:2; Hab 1:2-4“Ingawa ninalia, ‘Nimetendewa mabaya!’ sipati jibu;

ingawa ninaomba msaada, hakuna haki.

19:8 Mao 3:7; Hos 2:6; Mhu 6:4; Yer 14:19Yeye ameizuia njia yangu hivyo siwezi kupita;

ameyafunika mapito yangu na giza.

19:9 Ay 12:17; Za 89:39-44; Mao 5:16Amenivua heshima yangu,

na kuniondolea taji kichwani pangu.

19:10 Ay 12:14; 7:6; 14:7Amenibomoa kila upande hadi nimeisha;

amelingʼoa tegemeo langu kama mti.

19:11 Ay 16:9; 13:14Hasira yake imewaka juu yangu;

amenihesabu kuwa miongoni mwa adui zake.

19:12 Ay 16:13; 16:10; 3:23Majeshi yake yananisogelea kwa nguvu;

yamenizingira,

yamepiga kambi kulizunguka hema langu.

19:13 Ay 16:10-13; 30:12; Mt 26:56; 2Tim 4:16“Amewatenga ndugu zangu mbali nami;

wale tunaojuana nao wamefarakana nami kabisa.

19:14 Ay 19:19; 2Sam 15:12; Ay 12:4; 16:20; Za 88:18; Yer 20:10; 38:22Watu wa jamaa yangu wamekwenda mbali;

rafiki zangu wamenisahau.

19:15 Mwa 14:14; Mhu 2:7Wageni wangu na watumishi wangu wa kike wananiona kama mgeni;

wananitazama kama mgeni.

Namwita mtumishi wangu, wala haitiki,

ingawa namwomba kwa kinywa changu mwenyewe.

19:17 Za 38:5Pumzi ya kinywa changu ni kinyaa kwa mke wangu;

nimekuwa chukizo mno kwa ndugu zangu mwenyewe.

19:18 2Fal 2:23; Ay 13:25Hata watoto wadogo hunidhihaki;

ninapojitokeza, hunifanyia mzaha.

19:19 Za 38:11; 55:12-13; Ay 3:10Rafiki zangu wa moyoni wote wananichukia kabisa;

wale niwapendao wamekuwa kinyume nami.

19:20 Ay 2:5Mimi nimebaki mifupa na ngozi tu;

nimeponea nikiwa karibu kufa.

19:21 Ay 6:14; Amu 2:15; Ay 4:5; 10:3; Mao 3:1“Nihurumieni, rafiki zangu, kuweni na huruma,

kwa kuwa mkono wa Mungu umenipiga.

19:22 Ay 13:25; 16:11; Mit 30:14; Isa 53:4Kwa nini mnanifuatia kama Mungu afanyavyo?

Hamtosheki kamwe na mwili wangu?

19:23 Kut 17:16; Isa 30:8“Laiti maneno yangu yangewekwa kwenye kumbukumbu,

laiti kwamba yangeandikwa kwenye kitabu,

19:24 Yer 17:1; Ay 16:18kwamba yangechorwa kwenye risasi kwa kifaa cha chuma,

au kuyachonga juu ya mwamba milele!

19:25 Law 25:25; Mit 23:11; 1Sam 14:39; Ay 16:19Ninajua kwamba Mkombozi19:25 Au: Mtetezi. wangu yu hai,

naye kwamba mwishoni atasimama juu ya nchi.

19:26 Hes 12:8; 1Yn 3:2Nami baada ya ngozi yangu kuharibiwa,

bado nikiwa na mwili huu nitamwona Mungu;

19:27 Lk 2:30; Za 42:1; 63:1; 54:2mimi nitamwona kwa macho yangu mwenyewe:

mimi, wala si mwingine.

Tazama jinsi moyo wangu unavyomtamani sana!

“Kama mkisema, ‘Tazama tutakavyomwinda,

maadamu mzizi wa tatizo uko ndani yake,’

19:29 Ay 15:22; Za 58:11; Mhu 12:14ninyi wenyewe uogopeni upanga,

kwa kuwa ghadhabu italeta adhabu kwa upanga,

nanyi ndipo mtakapojua kwamba kuna hukumu.”

Read More of Ayubu 19

Ayubu 20:1-29

Sofari Anasema: Uovu Hupokea Malipo Ya Haki

20:1 Ay 2:11Ndipo Sofari Mnaamathi akajibu:

20:2 Za 42:5; Mao 1:20“Mawazo yanayonisumbua yananisukuma kujibu,

kwa sababu nimehangaika sana.

20:3 Ay 19:3Ninasikia makaripio ambayo yananivunjia heshima,

nao ufahamu wangu unanisukuma kujibu.

20:4 Kum 4:32; Ay 32:7“Hakika unajua jinsi ilivyokuwa tangu zamani,

tangu zamani mwanadamu alipowekwa duniani,

20:5 Ay 8:12; Za 73:19; 37:35macheko ya mtu mwovu ni ya muda mfupi,

nayo furaha ya wasiomcha Mungu hudumu kwa kitambo tu.

20:6 Ay 33:17; Isa 16:6; Mwa 11:4; Isa 14:13-14; Oba 1:3-4Ingawa kujikweza kwake hufikia mbinguni

na kichwa chake hugusa mawingu,

20:7 Ay 4:20; 7:8; 14:20ataangamia milele kama mavi yake mwenyewe.

Wale waliomwona watauliza, ‘Yuko wapi?’

20:8 Za 90:5; 73:20; Mhu 6:12; 12:7; Ay 18:11-18; Isa 17:14; 29:7Kama ndoto hutoweka, wala hapatikani tena,

amefukuziwa mbali kama maono ya usiku.

20:9 Ay 7:8Jicho lililomwona halitamwona tena;

mahali pake hapatamwona tena.

20:10 Ay 5:4; 20:15, 18, 20; 3:15Watoto wake watalipa yote baba yao aliyowadhulumu maskini,

nayo mikono yake itarudisha mali yote aliyonyangʼanya watu.

20:11 Ay 13:26; 21:24; 17:16Nguvu za ujana zilizoijaza mifupa yake,

zitalala naye mavumbini.

20:12 Ay 15:16; Za 10:7; 140:3“Ingawa uovu ni mtamu kinywani mwake

naye huuficha chini ya ulimi wake,

20:13 Hes 11:18-20ingawa hawezi kukubali kuuachia uende,

lakini huuweka kinywani mwake.

20:14 Za 104:26; Ay 10:18; Mwa 1:21; Ay 41:1, 8, 10, 2520:14 Mit 20:17; Yer 2:19; 4:18; Ufu 10:9; Hes 21:6Hata hivyo chakula chake kitakuwa kichungu tumboni mwake,

nacho kitakuwa sumu kali ya nyoka ndani yake.

20:15 Ay 20:10; Law 18:25Atatema mali alizozimeza;

Mungu atalifanya tumbo lake kuzitapika.

20:16 Kum 32:24, 34Atanyonya sumu za majoka;

meno ya nyoka mwenye sumu kali yatamuua.

20:17 Kum 32:13-14; Ay 29:6; Yer 17:6Hatafurahia vijito,

mito inayotiririsha asali na siagi.

20:18 Ay 20:10; 5:5; Za 109:11Vile alivyovitaabikia atavirudisha bila kuvila;

hatafurahia faida itokanayo na biashara yake.

20:19 Kum 15:11; Amo 8:4Kwa kuwa aliwaonea maskini na kuwaacha pasipo kitu;

amenyangʼanya kwa nguvu nyumba asizozijenga.

20:20 Mhu 5:12-14“Hakika hatakuwa na raha katika kutamani kwake sana;

hawezi kujiokoa mwenyewe kwa hazina zake.

20:21 Ay 7:8Hakuna chochote kitakachosalia kwa ajili yake ili ale;

kufanikiwa kwake hakutadumu.

20:22 Amu 2:15; Lk 2:16-20; Ay 20:29; 21:17, 30; 31:2-3Katikati ya wingi wa ustawi wake, dhiki itampata;

taabu itamjia kwa nguvu zote.

20:23 Za 78:30-31Atakapokuwa amelijaza tumbo lake,

Mungu ataionyesha ghadhabu kali dhidi yake,

na kumnyeshea mapigo juu yake.

20:24 Yer 46:21; Amo 5:19; Isa 24:18Ijapokuwa aikimbia silaha ya chuma,

mshale wa shaba utamchoma.

20:25 Ay 18:11; 16:13; Za 88:15-16Atauchomoa katika mgongo wake,

ncha ingʼaayo kutoka ini lake.

Vitisho vitakuja juu yake;

20:26 Ay 5:14; 1:16; 15:34; 26:6; 28:22; 31:12; Za 21:9giza nene linavizia hazina zake.

Moto usiopepewa na mtu utamteketeza,

na kuangamiza yaliyosalia nyumbani mwake.

20:27 Kum 31:28; Isa 26:21Mbingu zitaweka wazi hatia yake,

nayo nchi itainuka kinyume chake.

20:28 Kum 28:31; Mt 7:26-27; Hes 14:28-32; Efe 5:6Mafuriko yataichukua nyumba yake,

maji yaendayo kasi katika siku ya ghadhabu ya Mungu.

20:29 Yer 13:25; Kum 29:20, 28; Ufu 21:8; Mt 24:51Hili ndilo fungu Mungu alilowagawia waovu,

urithi uliowekwa kwa ajili yao na Mungu.”

Read More of Ayubu 20

Ayubu 21:1-34

Hotuba Ya Saba Ya Ayubu

Ayubu Anajibu: Waovu Mara Nyingi Huenda Bila Kuadhibiwa

Ndipo Ayubu akajibu:

21:2 Ay 13:17; 21:34“Yasikilizeni maneno yangu kwa makini;

hii na iwe faraja mnayonipa mimi.

21:3 Ay 6:14; 11:3; 16:10Nivumilieni ninapozungumza,

nami nikishazungumza, endeleeni kunidhihaki.

21:4 Za 22:1-3; Ay 6:3, 11; 1Sam 1:16“Je, kwani malalamiko yangu yanaelekezwa kwa mwanadamu?

Kwa nini nisikose subira?

21:5 Amu 18:19; Ay 40:4Niangalieni mkastaajabu;

mkaweke mkono juu ya vinywa vyenu.

21:6 Mwa 45:3; Ay 4:14Ninapowaza juu ya hili, ninaogopa,

nao mwili wangu unatetemeka.

21:7 Mhu 7:15; Mal 3:15; Yer 12:1-3Kwa nini waovu wanaendelea kuishi,

wakifikia umri wa uzee na kuendelea kuwa na nguvu?

21:8 Za 17:14; Mal 3:15Huwaona watoto wao wakithibitika

wakiwa wamewazunguka,

wazao wao mbele za macho yao.

21:9 Ay 5:24; Za 73:5Nyumba zao zi salama wala hakuna hofu;

fimbo ya Mungu haiko juu yao.

21:10 Kut 23:26Madume yao ya ngʼombe huvyaza bila kushindwa kamwe;

ngʼombe wao huzaa wala hawaharibu mimba.

21:11 Za 78:52; 107:41Huwatoa watoto wao nje kama kundi;

wadogo wao huchezacheza.

21:12 1Nya 15:16; Mt 15:17Huimba nyimbo kwa matari na kwa kinubi,

nao huifurahia sauti ya filimbi.

21:13 Ay 24:19; Za 49:14; Isa 14:15; Ay 3:13Huitumia miaka yao katika mafanikio

nao hushuka kaburini kwa amani.

21:14 Ay 4:17; Kum 32:15; Isa 30:11; 1Sam 11:15Lakini humwambia Mungu, ‘Tuache sisi!’

Hatuna haja ya kufahamu njia zako.

21:15 Yer 9:6; Mal 3:14Mwenyezi ni nani hata tumtumikie?

Tutapata faida gani kumwomba?

21:16 Ay 22:18; Za 1:1; 26:5; 36:1Lakini kufanikiwa kwao hakupo mikononi mwao wenyewe,

hivyo najitenga mbali na shauri la waovu.

21:17 Ay 18:5; 18:12; 20:22, 28“Lakini ni mara ngapi taa ya waovu huzimwa?

Ni mara ngapi maafa huwajia,

yale yawapatayo ambayo Mungu

huwapangia katika hasira yake?

21:18 Ay 13:15; Mwa 19:15; Ay 7:10; Mit 10:25; Mwa 7:23Ni mara ngapi huwa kama majani makavu mbele ya upepo,

kama makapi yachukuliwayo na dhoruba?

21:19 Kut 20:5; Yn 9:2Imesemekana, ‘Mungu huiweka akiba adhabu ya mtu

kwa ajili ya wanawe.’

Mungu na amlipe mtu mwenyewe,

ili apate kulijua!

21:20 Ay 6:4; Isa 51:17; Yer 25:15; Ufu 14:10Macho yake mwenyewe na yaone maangamizi yake;

yeye na ainywe ghadhabu ya Mwenyezi.

21:21 Ay 14:22; 14:5; 14:21; Mhu 9:5-6Kwani anajali nini kuhusu jamaa anayoiacha nyuma,

miezi yake aliyopangiwa ifikapo mwisho?

21:22 Za 94:12; 86:8; Rum 11:34“Je, yuko mtu yeyote awezaye kumfundisha Mungu maarifa,

iwapo yeye ndiye ahukumuye hata walio juu ya wote?

21:23 Mwa 15:15; Ay 13:26; 3:13Mtu mmoja hufa akiwa na nguvu zake kamili,

akiwa salama na mwenye raha kamili,

21:24 Mit 3:8mwili wake ukiwa umenawiri,

nayo mifupa yake ikiwa imejaa mafuta ndani yake.

21:25 Ay 10:1Mtu mwingine hufa katika uchungu wa nafsi,

akiwa hajafurahia kamwe jambo lolote zuri.

21:26 Mhu 9:2-3; Isa 14:11Hao wote hulala mavumbini,

nao mabuu huwafunika wote.

“Ninayajua kikamilifu yale mnayoyafikiri,

mipango ambayo kwayo mngenitendea mabaya.

21:28 Ay 1:3; 12:21; 29:25; 31:37; 8:22Mwasema, ‘Iko wapi sasa nyumba ya huyo mtu mkuu,

mahema ambayo watu waovu walikaa?’

Je, hamkuwahi kuwauliza hao wanaosafiri?

Je, hamkutafakari taarifa zao:

21:30 Ay 31:3; Mit 16:4; Isa 5:30; Rum 5:2kwamba mtu mwovu huepushwa kutoka siku ya maafa,

kwamba huokolewa kutoka siku ya ghadhabu?

21:31 Ay 34:11; Za 62:12; Mit 24:11-12; Isa 59:18Ni nani hulaumu matendo yake mbele ya uso wake?

Ni nani ampatilizaye kwa yale aliyoyatenda?

21:32 Isa 14:18Hupelekwa kaburini,

nao ulinzi ukawekwa kwenye kaburi lake.

21:33 Ay 3:17-19; 17:16; 24:24Udongo ulio bondeni ni mtamu kwake;

watu wote watamfuata,

nao umati wa watu usiohesabika umemtangulia.

“Hivyo ninyi mnawezaje kunifariji kwa upuzi wenu?

Hakuna kilichosalia cha majibu yenu isipokuwa uongo!”

Read More of Ayubu 21