2 Nyakati 35:20-27, 2 Nyakati 36:1-23 NEN

2 Nyakati 35:20-27

Kifo Cha Yosia

(2 Wafalme 23:28-30)

35:20 Isa 10:9; Yer 46:2; Mwa 2:14; 2Fal 23:29; 25:11Baada ya haya yote, Yosia alipomaliza kulitengeneza vizuri Hekalu, Neko mfalme wa Misri, akapanda ili kupigana huko Karkemishi katika Mto Frati, naye Yosia akatoka kwenda kupigana naye. 35:21 2Fal 18:25; Dan 4:35; 1Fal 13:18; Isa 36:10; Yer 25:9Lakini Neko akamtumia wajumbe kusema, “Kuna ugomvi gani kati yangu mimi na wewe, Ee Mfalme wa Yuda? Si wewe ninayekushambulia wakati huu, bali ile nyumba ambayo nina vita nayo, Mungu ameniambia niharakishe, kwa hivyo acha kumpinga Mungu, ambaye yuko pamoja nami, la sivyo atakuangamiza.”

35:22 Amu 5:19; 1Sam 28:8; 1Fal 22:30; 14:2; 2Nya 18:29Lakini hata hivyo, Yosia hakukubali kumwacha, bali alijibadilisha ili kupigana naye vita. Hakusikiliza yale Neko aliyokuwa amemwambia kwa agizo la Mungu bali alikwenda kupigana naye katika tambarare ya Megido.

35:23 1Fal 22:34; Dan 2:21Wapiga upinde wakampiga Mfalme Yosia, naye akawaambia maafisa wake, “Niondoeni, nimejeruhiwa vibaya sana.” 35:24 2Fal 23:30; Zek 12:11Kwa hiyo wakamshusha kutoka kwenye gari lake la farasi, wakamweka kwenye gari lingine alilokuwa nalo na kumleta Yerusalemu, ambako alifia. Akazikwa katika makaburi ya baba zake, nayo Yuda yote na Yerusalemu wakamwombolezea Yosia.

35:25 Mwa 50:10; Yer 22:10-16; Mao 4:20; Mt 9:23; Amo 5:16; Mhu 12:5; Yer 9:17Nabii Yeremia akatunga maombolezo kwa ajili ya kifo chake, nao waimbaji wote, wanaume kwa wanawake, hufanya ukumbusho wa Yosia katika maombolezo hadi leo. Haya yakafanywa desturi katika Israeli, nayo yameandikwa katika Maombolezo.

35:26 Za 112:6; Mit 10:7; 22:1Matukio mengine ya utawala wa Yosia na matendo yake mema, kulingana na yale yaliyoandikwa katika sheria ya Bwana: matukio yote, kuanzia mwanzo hadi mwisho, yameandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli na Yuda.

Read More of 2 Nyakati 35

2 Nyakati 36:1-23

Mfalme Yehoahazi Wa Yuda

(2 Wafalme 23:30-35)

36:1 2Fal 23:30; 2Nya 33:25Watu wa nchi wakamchukua Yehoahazi mwana wa Yosia na kumfanya mfalme mahali pa baba yake huko Yerusalemu.

Yehoahazi alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitatu alipoanza kutawala, akatawala huko Yerusalemu kwa miezi mitatu. Mfalme wa Misri akamwondoa madarakani huko Yerusalemu na akatoza Yuda kodi ya talanta 10036:3 Talanta 100 za fedha ni sawa na tani 3.75. za fedha na talanta moja36:3 Talanta moja ya dhahabu ni sawa na kilo 34. ya dhahabu. 36:4 Yer 22:10-12; Eze 19:3Mfalme wa Misri akamweka Eliakimu, nduguye Yehoahazi, kuwa mfalme juu ya Yuda na Yerusalemu na kubadili jina la Eliakimu kuwa Yehoyakimu. Lakini Neko akamchukua Yehoahazi, Nduguye Eliakimu akampeleka Misri.

Yehoyakimu Mfalme Wa Yuda

(2 Wafalme 23:35–24:7)

36:5 Yer 25:1; 36:1, 27-32; 2Fal 23:36-37Yehoyakimu alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na mmoja. Akafanya maovu machoni pa Bwana Mungu wake. 36:6 Yer 25:9; Eze 29:18; 19:9; 2Fal 24:1-6; Hab 1:6-10Nebukadneza mfalme wa Babeli akamshambulia na kumfunga kwa pingu za shaba akampeleka Babeli. 36:7 2Fal 24:13; Yer 27:16Nebukadneza akachukua pia vyombo kutoka Hekalu la Bwana na kuviweka katika hekalu lake36:7 Au: katika jumba lake la kifalme. huko Babeli.

36:8 1Nya 3:16Matukio mengine ya utawala wa Yehoyakimu, machukizo aliyoyafanya na yote yaliyoonekana dhidi yake, yameandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli na Yuda. Naye Yehoyakini mwanawe akawa mfalme baada yake.

Yehoyakini Mfalme Wa Yuda

(2 Wafalme 24:8-17)

36:9 2Fal 24:8; Yer 24:1; 27:16Yehoyakini alikuwa na miaka kumi na minane alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miezi mitatu na siku kumi. Akafanya yaliyo maovu machoni pa Bwana. 36:10 Isa 52:11; Dan 5:2Mnamo majira ya vuli, Mfalme Nebukadneza akatuma watu, nao wakamleta Babeli, pamoja na vyombo vya thamani kutoka Hekalu la Bwana. Naye akamfanya Sedekia, ndugu yake Yehoyakimu kuwa mfalme wa Yuda na Yerusalemu.

Mfalme Sedekia Wa Yuda

(2 Wafalme 24:18-20; Yeremia 52:1-3)

36:11 2Fal 24:17; Yer 39:1Sedekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mmoja alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka kumi na mmoja. 36:12 Yer 39:18; Kum 8:3; Yer 21:3-7Alifanya maovu machoni pa Bwana Mungu wake, wala hakujinyenyekeza mbele ya nabii Yeremia, ambaye alinena neno la Bwana. 36:13 Eze 17:13; Kut 32:9; 2Fal 17:14; Neh 8:16-17; Yer 52:3; Kut 17:15Pia alimwasi Mfalme Nebukadneza, ambaye alikuwa amemwapisha kwa jina la Mungu. Akashupaza shingo na akafanya moyo wake kuwa mgumu wala hakutaka kumgeukia Bwana, Mungu wa Israeli. 36:14 1Nya 5:25Zaidi ya hayo viongozi wote wa makuhani pamoja na watu wakazidi kukosa uaminifu zaidi na zaidi, wakafanya machukizo yote kama walivyofanya mataifa wakinajisi Hekalu la Bwana alilokuwa amelitakasa huko Yerusalemu.

Kuanguka Kwa Yerusalemu

(2 Wafalme 25:1-21; Yeremia 52:3-11)

36:15 Hag 1:13; Yer 11:7; 44:4-6; Hos 11:8; Yer 25:3Bwana, Mungu wa baba zao, akawapelekea neno kupitia wajumbe wake tena na tena, kwa sababu alikuwa anawahurumia watu wake pamoja na mahali pa maskani yake. 36:16 Mit 1:25-31; Mik 2:11; Yer 7:26; Dan 9:6; Lk 16:14Lakini waliwadhihaki wajumbe wa Bwana wakayadharau maneno yake na kuwacheka manabii wake mpaka ghadhabu ya Bwana ikawa kubwa dhidi ya watu wake na hakukuwa na namna ya kuituliza. 36:17 Yer 9:21; 18:21; Mao 2:21; Eze 9:6Mungu akamwinua dhidi yao mfalme wa Wakaldayo, aliyewaua vijana wao wa kiume kwa upanga ndani ya mahali patakatifu, ambaye hakumbakiza kijana mwanaume wala kijana mwanamke, wazee wala vikongwe. Mungu akawatia wote mikononi mwa Nebukadneza. 36:18 Yer 17:20; 2Fal 25:13Akavichukua kwenda Babeli vyombo vyote kutoka Hekalu la Mungu, vikubwa na vidogo, hazina za Hekalu la Bwana pamoja na hazina za mfalme na za maafisa wake. 36:19 Amo 2:5; 1Fal 9:8-9; 14:13; Mao 2:6; Za 79:1-3Wakalichoma Hekalu la Mungu na kuzibomoa kuta za Yerusalemu, wakachoma moto majumba yote ya kifalme na kuharibu kila kitu chake cha thamani.

36:20 Ezr 2:1; Neh 7:6; Yer 27:7Wale watu walionusurika kuuawa kwa upanga wakachukuliwa kwenda uhamishoni Babeli. Nao wakawa watumishi wake na wa wanawe mpaka wakati wa utawala wa ufalme wa Uajemi ulifika. 36:21 Law 25:4; 26:34Nchi ikaendelea kufurahia pumziko lake la Sabato, wakati wote wa kufanywa kwake ukiwa ilipumzika mpaka ile miaka sabini ilipotimia katika kutimiza neno la Bwana lililonenwa na Yeremia.

Koreshi Atangaza Uhuru Kwa Waliokuwa Uhamishoni

(Ezra 1:1-4)

36:22 Yer 29:10; Isa 44:28Katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Koreshi mfalme wa Uajemi, ili kulitimiza neno la Bwana lililosemwa na nabii Yeremia, Bwana aliusukuma moyo wa Koreshi mfalme wa Uajemi kutangaza katika himaya yake yote kwa maandishi:

“Hili ndilo asemalo Koreshi mfalme wa Uajemi:

“ ‘Bwana, Mungu wa mbinguni, amenipa falme zote duniani, na ameniagiza kumjengea Hekalu huko Yerusalemu katika Yuda. Yeyote wa watu wake miongoni mwenu, Mungu wake na awe pamoja naye, wacha huyo mtu na apande.’ ”

Read More of 2 Nyakati 36