Zaburi 89:46-52
89:46 Za 79:5Hata lini, Ee Bwana? Utajificha milele?
Ghadhabu yako itawaka kama moto hata lini?
89:47 Mwa 47:9; Ay 7:7; Za 39:5; 1Pet 1:24Kumbuka jinsi maisha yangu yanavyopita haraka.
Ni kwa ubatili kiasi gani umemuumba mwanadamu!
89:48 Mwa 5:24; Za 22:29; Ebr 11:5Ni mtu gani awezaye kuishi na asione kifo,
au kujiokoa mwenyewe kutoka nguvu za kaburi?89:48 Kaburi hapa maana yake ni Kuzimu, kwa Kiebrania ni Sheol.
89:49 2Sam 7:12; Isa 55:13Ee Bwana, uko wapi upendo wako mkuu wa mwanzoni,
ambao katika uaminifu wako ulimwapia Daudi?
89:50 Za 69:19Bwana kumbuka jinsi mtumishi wako amesimangwa,
jinsi ninavyovumilia moyoni mwangu dhihaka za mataifa yote,
89:51 Za 74:10dhihaka ambazo kwazo adui zako
wamenisimanga, Ee Bwana,
ambazo kwazo wamesimanga
kila hatua ya mpakwa mafuta wako.
89:52 Za 41:13; 72:19Msifuni Bwana milele!
Amen na Amen.