Zaburi 89:38-45
89:38 1Nya 28:9; Isa 22:5; Mao 2:2Lakini wewe umemkataa, umemdharau,
umemkasirikia sana mpakwa mafuta wako.
89:39 Mao 5:16Umelikana agano lako na mtumishi wako,
na umeinajisi taji yake mavumbini.
89:40 Za 80:12; Isa 22:5; Mao 2:2Umebomoa kuta zake zote,
na ngome zake zote umezifanya kuwa magofu.
89:41 Amu 2:14; Za 44:13Wote wapitao karibu wamemnyangʼanya mali zake;
amekuwa dharau kwa jirani zake.
89:42 Za 13:2; 80:6Umeutukuza mkono wa kuume wa adui zake,
umewafanya watesi wake wote washangilie.
89:43 Za 44:10Umegeuza makali ya upanga wake,
na hukumpa msaada katika vita.
Umeikomesha fahari yake,
na kukiangusha kiti chake cha enzi.
89:45 Za 39:5; 44:15; 109:29Umezifupisha siku za ujana wake,
umemfunika kwa vazi la aibu.