Zaburi 88:9-18
88:9 Za 38:10; 5:2; 143:6; Ay 11:13nuru ya macho yangu
imefifia kwa ajili ya huzuni.
Ee Bwana, ninakuita kila siku,
ninakunyooshea wewe mikono yangu.
88:10 Za 6:5Je, wewe huwaonyesha wafu maajabu yako?
Je, wale waliokufa huinuka na kukusifu?
88:11 Za 30:9Je, upendo wako hutangazwa kaburini,
uaminifu wako katika Uharibifu?88:11 Yaani Abadon.
88:12 Ay 10:21; 31:12; Mhu 8:10Je, maajabu yako hujulikana mahali pa giza,
au matendo yako ya haki katika nchi ya usahaulifu?
88:13 Za 30:2; 5:3; 55:17; 119:147Lakini ninakulilia wewe, Ee Bwana, unisaidie;
asubuhi maombi yangu huja mbele zako.
88:14 Za 43:2; 13:1Ee Bwana, kwa nini unanikataa
na kunificha uso wako?
88:15 Dan 9:26; Za 9:12; 129:1; Yer 22:21; Eze 16:22; Hos 2:15; Isa 53:8; Ay 6:4; 18:11; 2Kor 4:8Tangu ujana wangu nimeteseka, nikakaribia kifo;
nimepatwa na hofu zako, nami nimekata tamaa.
88:16 Za 7:11; Ay 6:4Ghadhabu yako imepita juu yangu;
hofu zako zimeniangamiza.
88:17 Za 124:4Mchana kutwa zinanizunguka kama mafuriko;
zimenimeza kabisa.
88:18 Za 88:8; 38:11; Ay 19:13Umeniondolea marafiki na wapendwa wangu;
giza limekuwa ndilo rafiki yangu wa karibu kuliko wote.