Zaburi 88:1-9
Zaburi 88
Kilio Kwa Ajili Ya Kuomba Msaada
Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Kwa mwimbishaji. Mtindo wa mahalathi leanothi. Utenzi wa Hemani Mwezrahi.
88:1 Za 51:14; 3:4; 22:2; Lk 18:7Ee Bwana, Mungu uniokoaye,
nimelia mbele zako usiku na mchana.
Maombi yangu yafike mbele zako,
utegee kilio changu sikio lako.
88:3 Ay 33:22; Isa 38:10; Za 6:3; 25:17; 107:18Kwa maana nafsi yangu imejaa taabu,
na maisha yangu yanakaribia kaburi.88:3 Kaburi hapa maana yake ni Kuzimu, kwa Kiebrania ni Sheol.
88:4 Za 31:12; 18:1Nimehesabiwa miongoni mwa wale waendao shimoni,
niko kama mtu asiye na nguvu.
88:5 Za 31:22Nimetengwa pamoja na wafu,
kama waliochinjwa walalao kaburini,
ambao huwakumbuki tena,
ambao wamekatiliwa mbali na uangalizi wako.
88:6 Za 30:1; 69:15; Mao 3:55; Yon 2:3Umenitupa katika shimo lenye kina kirefu sana,
katika vina vya giza nene.
88:7 Za 7:11; 42:7Ghadhabu yako imekuwa nzito juu yangu,
umenigharikisha kwa mawimbi yako yote.
88:8 Ay 3:23; 19:13; Za 31:11; Yer 32:2; 33:1Umenitenga na rafiki zangu wa karibu
na kunifanya chukizo kwao.
Nimezuiliwa, wala siwezi kutoroka;
88:9 Za 38:10; 5:2; 143:6; Ay 11:13nuru ya macho yangu
imefifia kwa ajili ya huzuni.
Ee Bwana, ninakuita kila siku,
ninakunyooshea wewe mikono yangu.