Zaburi 86:1-10
Zaburi 86
Kuomba Msaada
Maombi ya Daudi.
86:1 Za 17:6Ee Bwana, sikia na unijibu,
kwa maana mimi ni maskini na mhitaji.
86:2 Za 25:2; 31:14Linda maisha yangu, kwa maana nimejiweka kwako,
wewe ni Mungu wangu,
mwokoe mtumishi wako anayekutumaini.
86:3 Za 4:1; 9:13; 57:1; 88:9Ee Bwana, nihurumie mimi,
kwa maana ninakuita mchana kutwa.
86:4 Za 46:5; 143:8Mpe mtumishi wako furaha,
kwa kuwa kwako wewe, Ee Bwana,
ninainua nafsi yangu.
86:5 Yoe 2:13; Yon 4:2; Neh 9:17; Za 103:8; 145:8; 130:7, 8; Kut 34:6Ee Bwana, wewe ni mwema na mwenye kusamehe,
umejaa upendo kwa wote wakuitao.
86:6 Za 5:2; 17:1Ee Bwana, sikia maombi yangu,
sikiliza kilio changu unihurumie.
86:7 Za 3:4; 4:3; 27:5; 50:15; 94:13; 80:18; 91:15; Isa 30:19; 58:9; 65:24; Ay 22:27; Zek 13:9; Hab 3:16Katika siku ya shida yangu nitakuita,
kwa maana wewe utanijibu.
86:8 Ay 21:22; Za 18:31; 1Sam 2:2; Kut 8:10; 15:11; Kum 3:24; 2Sam 7:22Ee Bwana, katikati ya miungu hakuna kama wewe,
hakuna matendo ya kulinganishwa na yako.
86:9 Za 65:2; 66:4; Isa 19:21; 27:13; 49:7; Zek 8:20-22; 14:6; Ufu 15:4; Isa 43:7; 44:23; Za 95:6, 7Ee Bwana, mataifa yote uliyoyafanya
yatakuja na kuabudu mbele zako;
wataliletea utukufu jina lako.
86:10 2Sam 7:22; Kut 3:20; Kum 6:4; Za 48:1; 71:17; 72:18; 1Kor 8:4; Isa 37:16; 43:10; Mk 12:29; Efe 4:6Kwa maana wewe ni mkuu, na unafanya mambo ya ajabu;
wewe peke yako ndiwe Mungu.