Zaburi 84:1-7
Zaburi 84
Kuionea Shauku Nyumba Ya Mungu
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya wana wa Kora.
84:1 Kum 33:27; Za 27:4; 43:3; 90:1; 132:5; 26:8; 27:4; Ebr 9:23; Ufu 21:2, 3Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote,
makao yako yapendeza kama nini!
84:2 Ay 19:27; Yos 3:10Nafsi yangu inatamani sana,
naam, hata kuona shauku,
kwa ajili ya nyua za Bwana;
moyo wangu na mwili wangu
vinamlilia Mungu Aliye Hai.
84:3 Za 2:6; 5:2; 43:4; Yer 44:11Hata shomoro amejipatia makao,
mbayuwayu amejipatia kiota
mahali awezapo kuweka makinda yake:
mahali karibu na madhabahu yako,
Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote,
Mfalme wangu na Mungu wangu.
Heri wale wanaokaa nyumbani mwako,
wanaokusifu wewe daima.
84:5 Za 81:1; Yer 31:6Heri wale ambao nguvu zao ziko kwako,
na njia ziendazo Sayuni zimo mioyoni mwao.
84:6 Ay 38:26; Yoe 2:23Wanapopita katika Bonde la Baka,84:6 Yaani Bonde la Vilio.
hulifanya mahali pa chemchemi,
pia mvua za vuli hulijaza kwa madimbwi.84:6 Au: baraka.
84:7 Ay 17:9; Kum 16:16; 1Fal 8:1Huendelea toka nguvu hadi nguvu,
hadi kila mmoja afikapo
mbele za Mungu huko Sayuni.