Zaburi 81:8-16
81:8 Za 50:7; 78:1“Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya:
laiti kama mngenisikiliza, ee Israeli!
81:9 Kut 20:3Hamtakuwa na mungu mgeni miongoni mwenu;
msimsujudie mungu wa kigeni.
81:10 Kut 6:6; 13:3; 29:46; Eze 2:8; Za 107:9; 37:3; Yn 13:7Mimi ni Bwana Mungu wako,
niliyekutoa nchi ya Misri.
Panua sana kinywa chako
nami nitakijaza.
81:11 Kut 32:1-6“Lakini watu wangu hawakutaka kunisikiliza;
Israeli hakutaka kunitii.
81:12 Eze 20:25; Mdo 7:42; Rum 1:24Basi niliwaacha katika ukaidi wa mioyo yao
wafuate mashauri yao wenyewe.
81:13 Kum 5:29; Isa 48:18; Yer 44:4, 5; Mt 23:37“Laiti kama watu wangu wangalinisikiliza,
kama Israeli wangalifuata njia zangu,
81:14 Za 47:3; Amo 1:8ningaliwatiisha adui zao kwa haraka,
na kuugeuza mkono wangu dhidi ya watesi wao!
81:15 2Sam 22:45Wale wanaomchukia Bwana wangalinyenyekea mbele zake,
na adhabu yao ingedumu milele.
81:16 Kum 32:14Bali ninyi mngalilishwa ngano iliyo bora,
na kuwatosheleza kwa asali itokayo kwenye mwamba.”