Zaburi 80:8-19 NEN

Zaburi 80:8-19

80:8 Isa 5:1-2, 7; Yer 2:21; Mt 21:33-41; Kut 15:17; 23:28-30; Yos 13:6; Mdo 7:45; Eze 15:6Ulileta mzabibu kutoka Misri,

ukawafukuza mataifa, ukaupanda.

Uliandaa shamba kwa ajili yake,

mizizi ikawa imara, ukajaza nchi.

Milima ilifunikwa kwa kivuli chake,

matawi yake yakafunika mierezi mikubwa.

80:11 Kut 23:31; Za 72:8Matawi yake yalienea mpaka Baharini,80:11 Huenda inamaanisha Bahari ya Mediterania.

machipukizi yake mpaka kwenye Mto.80:11 Yaani Mto Frati.

80:12 Isa 5:5; 30:13; Za 89:40; Yer 39:8Mbona umebomoa kuta zake

ili wote wapitao karibu

wazichume zabibu zake?

80:13 Yer 5:6Nguruwe mwitu wanauharibu

na wanyama wa kondeni hujilisha humo.

80:14 Kum 26:15; Zek 1:12, 16, 17; Isa 63:15Turudie, Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote!

Tazama chini kutoka mbinguni na uone!

Linda mzabibu huu,

80:15 Isa 49:5mche ulioupanda kwa mkono wako wa kuume,

mwana uliyemlea

kwa ajili yako mwenyewe.

80:16 Za 79:1; Kum 28:20Mzabibu wako umekatwa, umechomwa moto,

unapowakemea, watu wako huangamia.

80:17 Ay 25:6; Za 89:21; 110:1; Kut 4:22; Dan 7:13, 14; Yn 5:21-27Mkono wako na utulie juu ya mtu aliyeko mkono wako wa kuume,

mwana wa mtu uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.

80:18 Za 85:6; Isa 57:15; Hos 6:2Ndipo hatutakuacha tena,

utuhuishe, nasi tutaliitia jina lako.

80:19 Hes 6:25; Za 27:4, 9Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe;

utuangazie uso wako,

ili tuweze kuokolewa.

Read More of Zaburi 80