Zaburi 80:1-7
Zaburi 80
Maombi Kwa Ajili Ya Kuponywa Kwa Taifa
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi za Agano.” Zaburi ya Asafu.
80:1 Kut 25:22; 1Sam 4:4; Za 77:20; 89:1; Kum 33:2Ee Mchungaji wa Israeli tusikie,
wewe umwongozaye Yosefu kama kundi;
wewe uketiye katika kiti cha enzi
katikati ya makerubi, angaza
80:2 Hes 2:18-24; Za 35:23; 54:1; 71:2; 109:26; 116:4; 119:94mbele ya Efraimu, Benyamini na Manase.
Uamshe nguvu zako,
uje utuokoe.
80:3 Za 71:20; 85:4; Yer 31:18; Mao 5:21; Hes 6:25; Za 80:7, 19; 1Fal 18:37Ee Mungu, uturejeshe,
utuangazie uso wako,
ili tuweze kuokolewa.
80:4 Za 74:10; Kum 29:20Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote,
hata lini hasira yako itawaka na kufoka moshi
dhidi ya maombi ya watu wako?
80:5 Ay 3:24; Isa 30:20Umewalisha kwa mkate wa machozi,
umewafanya wanywe machozi bakuli tele.
80:6 Za 79:4Tumekuwa chanzo cha ugomvi kwa jirani zetu,
na adui zetu wanatudhihaki.
80:7 Za 80:3Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe;
utuangazie uso wako,
nasi tuweze kuokolewa.