Zaburi 78:17-31
78:17 Za 78:32Lakini waliendelea kutenda dhambi dhidi yake,
wakiasi jangwani dhidi ya Aliye Juu Sana.
78:18 Kut 15:24; 17:2; 1Kor 10:9; Hes 11:4Kwa makusudi walimjaribu Mungu,
wakidai vyakula walivyovitamani.
78:19 Hes 11:4; 21:5Walinena dhidi ya Mungu, wakisema,
“Je, Mungu aweza kuandaa meza jangwani?
78:20 Hes 20:11; Kut 17:6Alipopiga mwamba, maji yalitoka kwa nguvu,
vijito vikatiririka maji mengi.
Lakini je, aweza kutupa chakula pia?
Je, anaweza kuwapa watu wake nyama?”
78:21 Hes 11:1Bwana alipowasikia, alikasirika sana,
moto wake ukawa dhidi ya Yakobo,
na ghadhabu yake ikawaka dhidi ya Israeli,
78:22 Kum 1:32; Ebr 3:19; 3:10kwa kuwa hawakumwamini Mungu,
wala kuutumainia ukombozi wake.
78:23 Mwa 7:11; Kum 28:12; 2Fal 7:2Hata hivyo alitoa amri kwa anga zilizo juu
na kufungua milango ya mbingu,
78:24 Kut 16:4; Yn 6:31; Neh 9:15, 20; 1Kor 10:3akawanyeshea mana ili watu wale;
aliwapa nafaka ya mbinguni.
Watu walikula mkate wa malaika,
akawatumia chakula chote ambacho wangeliweza kula.
78:26 Hes 11:31Aliachia upepo wa mashariki kutoka kwenye mbingu
na kuuongoza upepo wa kusini kwa uwezo wake.
78:27 Kut 16:13; Hes 11:31Aliwanyeshea nyama kama mavumbi,
ndege warukao kama mchanga wa pwani.
Aliwafanya washuke ndani ya kambi yao,
kuzunguka mahema yao yote.
78:29 Hes 11:20Walikula na kusaza,
kwa maana alikuwa amewapa kile walichotamani.
78:30 Hes 11:33Kabla hawajamaliza kula walichokitamani,
hata kilipokuwa kingali bado vinywani mwao,
78:31 Isa 10:16hasira ya Mungu ikawaka juu yao,
akawaua wale waliokuwa na nguvu zaidi miongoni mwao,
akiwaangusha vijana wa Israeli.