Zaburi 77:10-20 NEN

Zaburi 77:10-20

77:10 Ay 42:3; Za 31:22; Yer 10:19; Kut 15:6Ndipo nikawaza, “Huu ndio udhaifu wangu:

lakini nitakumbuka

miaka ya mkono wa kuume

wa Aliye Juu Sana.”

77:11 Neh 9:17; 1Nya 16:12; Za 28:5; Isa 5:14Nitayakumbuka matendo ya Bwana;

naam, nitaikumbuka miujiza yako ya zamani.

77:12 Mwa 24:63; Za 143:5Nitazitafakari kazi zako zote

na kuyawaza matendo yako makuu.

77:13 Za 73:17; 71:19; 86:8; Kut 15:11Ee Mungu, njia zako ni takatifu.

Ni mungu yupi aliye mkuu kama Mungu wetu?

77:14 Kut 3:20; 34:10Wewe ndiwe Mungu utendaye miujiza,

umeonyesha uwezo wako katikati ya mataifa.

77:15 Kut 6:6Kwa mkono wako wenye nguvu umewakomboa watu wako,

uzao wa Yakobo na Yosefu.

77:16 Kut 14:21, 28; Isa 50:2; Hab 3:8, 10; Yos 3:15, 16; Za 114:4Maji yalikuona, Ee Mungu,

maji yalikuona yakakimbia,

vilindi vilitetemeka.

77:17 Amu 5:4; Kut 9:23; Za 29:3; Kum 32:23Mawingu yalimwaga maji,

mbingu zikatoa ngurumo kwa radi,

mishale yako ikametameta huku na huko.

77:18 Za 55:8; 2Sam 22:13; Amu 5:4Ngurumo yako ilisikika katika upepo wa kisulisuli,

umeme wako wa radi ukaangaza dunia,

nchi ikatetemeka na kutikisika.

77:19 Hab 3:15; Kut 14:28; 14:22; Ay 9:8; 37:23Njia yako ilipita baharini,

mapito yako kwenye maji makuu,

ingawa nyayo zako hazikuonekana.

77:20 Kut 4:16; 13:21; Za 78:52; Isa 63:11; Hes 33:1Uliongoza watu wako kama kundi

kwa mkono wa Mose na Aroni.

Read More of Zaburi 77