Zaburi 77:10-20
77:10 Ay 42:3; Za 31:22; Yer 10:19; Kut 15:6Ndipo nikawaza, “Huu ndio udhaifu wangu:
lakini nitakumbuka
miaka ya mkono wa kuume
wa Aliye Juu Sana.”
77:11 Neh 9:17; 1Nya 16:12; Za 28:5; Isa 5:14Nitayakumbuka matendo ya Bwana;
naam, nitaikumbuka miujiza yako ya zamani.
77:12 Mwa 24:63; Za 143:5Nitazitafakari kazi zako zote
na kuyawaza matendo yako makuu.
77:13 Za 73:17; 71:19; 86:8; Kut 15:11Ee Mungu, njia zako ni takatifu.
Ni mungu yupi aliye mkuu kama Mungu wetu?
77:14 Kut 3:20; 34:10Wewe ndiwe Mungu utendaye miujiza,
umeonyesha uwezo wako katikati ya mataifa.
77:15 Kut 6:6Kwa mkono wako wenye nguvu umewakomboa watu wako,
uzao wa Yakobo na Yosefu.
77:16 Kut 14:21, 28; Isa 50:2; Hab 3:8, 10; Yos 3:15, 16; Za 114:4Maji yalikuona, Ee Mungu,
maji yalikuona yakakimbia,
vilindi vilitetemeka.
77:17 Amu 5:4; Kut 9:23; Za 29:3; Kum 32:23Mawingu yalimwaga maji,
mbingu zikatoa ngurumo kwa radi,
mishale yako ikametameta huku na huko.
77:18 Za 55:8; 2Sam 22:13; Amu 5:4Ngurumo yako ilisikika katika upepo wa kisulisuli,
umeme wako wa radi ukaangaza dunia,
nchi ikatetemeka na kutikisika.
77:19 Hab 3:15; Kut 14:28; 14:22; Ay 9:8; 37:23Njia yako ilipita baharini,
mapito yako kwenye maji makuu,
ingawa nyayo zako hazikuonekana.
77:20 Kut 4:16; 13:21; Za 78:52; Isa 63:11; Hes 33:1Uliongoza watu wako kama kundi
kwa mkono wa Mose na Aroni.