Zaburi 77:1-9
Zaburi 77
Matendo Makuu Ya Mungu Yanakumbukwa
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa Yeduthuni. Zaburi ya Asafu.
77:1 1Fal 8:52Nilimlilia Mungu ili anisaidie,
nilimlilia Mungu ili anisikie.
77:2 Mwa 37:35; 32:7; 2Sam 22:7; Za 118:5; 6:6; 22:2; 88:1; 50:15; Kut 9:29; Ay 11:13; Mt 2:18; Isa 26:9Nilipokuwa katika taabu, nilimtafuta Bwana,
usiku nilinyoosha mikono bila kuchoka
na nafsi yangu ilikataa kufarijika.
77:3 Za 6:6; 78:35; Kut 2:23; Yer 45:3; 6:2Ee Mungu, nilikukumbuka wewe, nikalia kwa huzuni;
nikatafakari, roho yangu ikadhoofika.
77:4 Za 39:2Ulizuia macho yangu kufumba;
nilikuwa nasumbuka, nikashindwa kusema.
77:5 Kum 32:7; Isa 51:9; Za 44:1; 143:5; Mhu 7:16Nilitafakari juu ya siku zilizopita,
miaka mingi iliyopita,
nilikumbuka nilivyoimba nyimbo usiku.
Moyo wangu ulitafakari
na roho yangu ikauliza:
77:7 Za 85:1; 102:13; 106:4; 1Nya 28:9“Je, Bwana atakataa milele?
Je, hatatenda mema tena?
77:8 Za 6:4; 90:14; 2Pet 3:9; Isa 27:11; Yn 2:4; Hes 23:19; Yer 15:18; Rum 9:6Je, upendo wake usio na mwisho umetoweka milele?
Je, ahadi yake imekoma nyakati zote?
77:9 Za 25:6; 40:11; 51:1; Isa 49:15Je, Mungu amesahau kuwa na huruma?
Je, katika hasira amezuia huruma yake?”