Zaburi 74:10-17
74:10 Za 6:3; 79:5; 80:4; 74:22; 44:16Ee Mungu, mtesi atakudhihaki mpaka lini?
Je, adui watalitukana jina lako milele?
74:11 Kut 15:6; Neh 5:13; Eze 5:3Kwa nini unazuia mkono wako,
mkono wako wa kuume?
Uutoe kutoka makunjo ya vazi lako
na uwaangamize!
74:12 Za 2:6; 24:7; 68:24; 44:4Lakini wewe, Ee Mungu, ni mfalme wangu tangu zamani,
unaleta wokovu duniani.
74:13 Isa 51:9; 27:1; Eze 29:3; 32:2; Kut 14:21Ni wewe uliyeigawanya bahari kwa uweza wako;
ulivunja vichwa vya wanyama wakubwa wa kutisha katika maji.
74:14 Hes 14:9; Za 72:9; Ay 3:8; Isa 13:21; 23:13; 34:14; Yer 50:39Ni wewe uliyeponda vichwa vya Lewiathani74:14 Lewiathani ni mnyama mkubwa wa baharini mwenye magamba anayefanana na joka kubwa, mwenye umbo la kutisha, asiyeweza kuvuliwa.
nawe ukamtoa kama chakula
kwa viumbe vya jangwani.
74:15 Kut 14:29; 17:6; Hes 20:11; Isa 11:16; Hab 3:9; Ufu 16:12; Yos 2:10Ni wewe uliyefungua chemchemi na vijito,
ulikausha mito ambayo ilikuwa ikitiririka daima.
74:16 Mwa 1:16; Za 136:7-9Mchana ni wako, nao usiku ni wako pia,
uliziweka jua na mwezi.
74:17 Mdo 17:26; Kum 32:8; Mwa 8:22Ni wewe uliyeiweka mipaka yote ya dunia,
ulifanya kiangazi na masika.