Zaburi 73:15-28 NEN

Zaburi 73:15-28

Kama ningesema, “Nitasema hivi,”

ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.

73:16 Mhu 8:17Nilipojaribu kuelewa haya yote,

yalikuwa magumu kwangu kuelewa.

73:17 Kut 15:17; Ay 8:13; Flp 3:19; Za 15:1; 77:13Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu,

ndipo nilipotambua mwisho wao.

73:18 Kum 32:35; Za 35:6; 17:13Hakika unawaweka mahali pa utelezi,

unawaangusha chini kwa uharibifu.

73:19 Kum 28:20; Mit 24:22; Isa 47:11; Mwa 19:15Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula,

wanatoweshwa kabisa na vitisho!

73:20 Za 78:65; Isa 29:8; Ay 20:8; Mit 12:11; 28:19Kama ndoto mtu aamkapo,

hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana,

utawatowesha kama ndoto.

Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa,

na roho yangu ilipotiwa uchungu,

73:22 Za 49:10; 92:6; 49:12, 20; Mhu 3:18; 9:12nilikuwa mpumbavu na mjinga,

nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.

73:23 Mwa 48:13Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote,

umenishika mkono wangu wa kuume.

73:24 Za 48:14; 1Fal 22:5; Isa 58:8; Yn 14:3; 2Kor 5:1Unaniongoza kwa shauri lako,

hatimaye utaniingiza katika utukufu.

73:25 Za 16:2; Flp 3:8Nani niliye naye mbinguni ila wewe?

Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.

73:26 Kum 32:9; Za 18:1; 84:2; 31:10; 40:12Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa,

bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu

na fungu langu milele.

73:27 Za 34:21; Law 6:2; Yer 5:11; Hos 4:12; 9:1Wale walio mbali nawe wataangamia,

unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.

73:28 Sef 3:2; Yak 4:8; Za 40:5; 26:7; 9:9; Ebr 10:22Lakini kwangu mimi,

ni vyema kuwa karibu na Mungu.

Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu;

nami nitayasimulia matendo yako yote.

Read More of Zaburi 73