Zaburi 71:1-8
Zaburi 71
Kuomba Ulinzi Na Msaada Siku Zote Za Maisha
71:1 Kum 23:15; Rut 2:12; Za 22:5Ee Bwana, nimekukimbilia wewe,
usiache nikaaibika kamwe.
71:2 2Fal 19:1671:2 Kut 34:6Kwa haki yako uniponye na kuniokoa,
unitegee sikio lako uniokoe.
71:3 Za 18:2Uwe kwangu mwamba wa kimbilio,
mahali nitakapokimbilia kila wakati;
toa amri ya kuniokoa, kwa kuwa wewe
ni mwamba wangu na ngome yangu.
71:4 2Fal 19:19; Za 140:4; Mwa 48:16Ee Mungu wangu uniokoe kutoka kwenye mkono wa mwovu,
kutoka kwenye makucha ya watu wabaya na wakatili.
71:5 Za 9:18; 25:5; Ay 4:6; Yer 17:7Kwa kuwa umekuwa tumaini langu, Ee Bwana Mwenyezi,
tegemeo langu tangu ujana wangu.
71:6 Ay 3:16; Za 9:1; 22:9; 34:1; 52:9; 119:164; 145:2Tangu kuzaliwa nimekutegemea wewe,
ulinitoa tumboni mwa mama yangu.
Nitakusifu wewe daima.
71:7 Kum 28:46; 1Kor 4:9; Za 61:3; 2Sam 22:3Nimekuwa kama kioja kwa wengi,
lakini wewe ni kimbilio langu imara.
71:8 Za 71:15; 51:15; 63:5; 96:6; 104:1Kinywa changu kimejazwa sifa zako,
nikitangaza utukufu wako mchana kutwa.