Zaburi 7:1-9
Zaburi 7
Sala Ya Mtu Anayedhulumiwa
Ombolezo la Daudi kwa Bwana kwa sababu ya Kushi, Mbenyamini.
7:1 Za 2:12; 11:1; 31:1; 3:7; 31:15; 119:86, 157, 161Ee Bwana, Mungu wangu, ninakukimbilia wewe,
uniokoe na kunikomboa na wote wanaonifuatia,
7:2 Mwa 49:9; Ufu 4:7; Za 3:2; 71:11; 1Pet 5:8la sivyo watanirarua kama simba
na kunichana vipande vipande, asiwepo wa kuniokoa.
7:3 Za 35:7, 19; Mit 24:28; 1Sam 24:7Ee Bwana, Mungu wangu, kama nimetenda haya
na kuna hatia mikononi mwangu,
7:4 Za 35:7, 19; Mit 24:28; 1Sam 24:7au ikiwa nimemtenda uovu aliye na amani nami,
au nimemnyangʼanya adui yangu pasipo sababu,
7:5 Kut 15:9; Ay 7:21; 2Sam 22:43; 2Fal 9:33; Isa 10:6; Mao 3:16basi adui anifuatie na kunipata,
auponde uhai wangu ardhini
na kunilaza mavumbini.
7:6 2Nya 6:41; Za 138:7; 35:23; 44:23; 94:2Amka kwa hasira yako, Ee Bwana,
inuka dhidi ya ghadhabu ya adui zangu.
Amka, Mungu wangu, uamue haki.
7:7 Za 68:18Kusanyiko la watu na likuzunguke.
Watawale kutoka juu.
7:8 1Nya 16:33; Mk 5:7; 1Sam 26:23; Za 18:20; Mwa 3:5; 20:5; Hes 24:16Bwana na awahukumu kabila za watu.
Nihukumu Ee Bwana,
kwa kadiri ya haki yangu,
kwa kadiri ya uadilifu wangu,
Ewe Uliye Juu Sana.
7:9 Yer 11:20; Ufu 2:23; Za 26:2; 37:23; 40:2; 1Sam 16:7; 1Nya 28:9Ee Mungu mwenye haki,
uchunguzaye mawazo na mioyo,
komesha ghasia za waovu
na ufanye wenye haki waishi kwa amani.