Zaburi 69:29-36
69:29 Za 20:1Mimi niko katika maumivu na dhiki;
Ee Mungu, wokovu wako na unihifadhi.
69:30 Za 28:7; 34:3Nitalisifu jina la Mungu kwa wimbo,
nami nitamtukuza kwa kumtolea shukrani.
69:31 Za 50:9-13; 51:16Hili litampendeza Bwana kuliko ngʼombe dume,
zaidi ya fahali akiwa na pembe na kwato zake.
69:32 Za 34:2; 22:26Maskini wataona na kufurahi:
ninyi mnaomtafuta Mungu, mioyo yenu na iishi!
69:33 Za 12:5Bwana huwasikia wahitaji
wala hadharau watu wake waliotekwa.
69:34 Za 96:11; 98:7; Isa 44:23Mbingu na dunia zimsifu,
bahari na vyote viendavyo ndani yake,
69:35 Oba 1:17; Ezr 9:9; Za 51:18kwa maana Mungu ataiokoa Sayuni
na kuijenga tena miji ya Yuda.
Kisha watu watafanya makao yao humo na kuimiliki,
69:36 Za 25:13; 37:29watoto wa watumishi wake watairithi
na wale wote walipendao jina lake
wataishi humo.