Zaburi 69:13-28
69:13 Isa 49:8; 2Kor 6:2; Za 17:7; 51:1Lakini Ee Bwana, ninakuomba,
kwa wakati ukupendezao;
katika upendo wako mkuu, Ee Mungu,
unijibu kwa wokovu wako wa hakika.
69:14 Za 69:2; 144:7Uniokoe katika matope,
usiniache nizame;
niokoe na hao wanichukiao,
kutoka kwenye vilindi vya maji.
69:15 Za 36:6; 68:22; Hes 21:33; Yer 22:2069:15 Za 28:1; 124:4, 5; Hes 16:33Usiache mafuriko yanigharikishe
au vilindi vinimeze,
au shimo lifumbe kinywa chake juu yangu.
69:16 Za 63:3Ee Bwana, unijibu, kwa wema wa upendo wako;
kwa huruma zako nyingi unigeukie.
69:17 Za 22:24; 143:7; 50:15; 66:14Usimfiche mtumishi wako uso wako,
uharakishe kunijibu, kwa sababu niko katika shida.
69:18 Za 49:15Njoo karibu uniokoe,
nikomboe kwa sababu ya adui zangu.
69:19 Za 22:6Unajua jinsi ninavyodharauliwa,
kufedheheshwa na kuaibishwa,
adui zangu wote unawajua.
69:20 Ay 16:2; Isa 63:5; Za 142:4Dharau zimenivunja moyo
na nimekata tamaa,
nimetafuta wa kunihurumia, lakini sikumpata,
wa kunituliza, lakini sikumpata.
69:21 Hes 6:3; Lk 23:36; Mt 27:34, 48; Mk 15:23, 36; Yn 19:28-30Waliweka nyongo katika chakula changu
na walinipa siki nilipokuwa na kiu.
69:22 1Sam 28:9; Ay 18:10Meza iliyoandaliwa mbele yao na iwe mtego,
nayo iwe upatilizo na tanzi.
69:23 Rum 11:9-10Macho yao yatiwe giza ili wasiweze kuona,
nayo migongo yao iinamishwe daima.
69:24 Za 79:6; Yer 10:25Uwamwagie ghadhabu yako,
hasira yako kali na iwapate.
69:25 Law 26:43; Mt 23:38; Mdo 1:20Mahali pao na pawe ukiwa,
wala asiwepo yeyote atakayeishi katika mahema yao.
69:26 Ay 19:22; Zek 1:15Kwa kuwa wanawatesa wale uliowajeruhi,
na kuzungumza juu ya maumivu ya wale uliowaumiza.
69:27 Neh 4:5; Za 109:14Walipize uovu juu ya uovu,
usiwaache washiriki katika wokovu wako.
69:28 Kut 32:32-33; Lk 10:20; Eze 13:9Wafutwe kutoka kitabu cha uzima
na wasiorodheshwe pamoja na wenye haki.