Zaburi 69:1-12 NEN

Zaburi 69:1-12

Zaburi 69

Kilio Cha Kuomba Msaada Wakati Wa Dhiki

Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi.” Zaburi ya Daudi.

69:1 Za 42:7; 32:6; Yon 2:5Ee Mungu, niokoe,

kwa maana maji yamenifika shingoni.

69:2 Ay 30:19Ninazama kwenye vilindi vya matope,

pasipo mahali pa kukanyaga,

Nimefika kwenye maji makuu,

mafuriko yamenigharikisha.

69:3 Za 6:6; 119:82Nimechoka kwa kuomba msaada,

koo langu limekauka.

Macho yangu yanafifia,

nikimtafuta Mungu wangu.

69:4 Yn 15:25; Za 25:19; 35:19; 38:19; 40:14; 119:95; Isa 32:7Wale wanaonichukia bila sababu

ni wengi kuliko nywele za kichwa changu;

wengi ni adui kwangu bila sababu,

wale wanaotafuta kuniangamiza.

Ninalazimishwa kurudisha

kitu ambacho sikuiba.

69:5 Za 38:5; 44:21Ee Mungu, wewe unajua upumbavu wangu,

wala hatia yangu haikufichika kwako.

Ee Bwana, ewe Bwana Mwenye Nguvu Zote,

wakutumainio wasiaibishwe

kwa ajili yangu;

wakutafutao wasifedheheshwe kwa ajili yangu,

Ee Mungu wa Israeli.

69:7 Yer 15:15; Za 39:8; 44:15Kwa maana nimestahimili dharau kwa ajili yako,

aibu imefunika uso wangu.

69:8 Ay 19:13-15; Za 31:11; 38:11; Isa 53:3; Yn 7:5Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu,

mgeni kwa wana wa mama yangu mwenyewe.

69:9 Yn 2:17; Rum 15:3; Za 89:50-51Kwa kuwa wivu wa nyumba yako unanila,

matukano ya wale wanaokutukana yameniangukia.

69:10 Za 35:13Ninapolia na kufunga,

lazima nivumilie matusi.

69:11 2Sam 3:31; Za 35:13Ninapovaa nguo ya gunia,

watu hunidharau.

69:12 Mwa 18:1; 23:10; Ay 30:9Wale wanaoketi mlangoni wananisimanga,

nimekuwa wimbo wa walevi.

Read More of Zaburi 69