Zaburi 68:7-14 NEN

Zaburi 68:7-14

68:7 Kut 13:21; Za 78:40; 106:14Ee Mungu, ulipowatangulia watu wako,

ulipopita nyikani,

68:8 2Sam 22:8; Amu 5:4, 5; Mhu 11:3; 2Sam 21:10; Kum 33:2dunia ilitikisika,

mbingu zikanyesha mvua,

mbele za Mungu, Yule wa Sinai,

mbele za Mungu, Mungu wa Israeli.

68:9 Kum 32:2; Ay 36:28; Eze 34:26Ee Mungu, ulinyesha mvua nyingi

na kuiburudisha ardhi iliyokuwa imechoka.

68:10 Kum 28:12; Za 65:9Ee Mungu, watu wako waliishi huko,

nawe kwa wingi wa utajiri wako

uliwapa maskini mahitaji yao.

68:11 Lk 2:13Bwana alitangaza neno,

waliolitangaza neno hilo walikuwa kundi kubwa:

68:12 Yos 10:16; Amu 5:30“Wafalme na majeshi walikimbia upesi,

watu waliobaki kambini waligawana nyara.

68:13 Mwa 49:14Hata ulalapo katikati ya mioto ya kambini,

mabawa ya njiwa wangu yamefunikwa kwa fedha,

manyoya yake kwa dhahabu ingʼaayo.”

68:14 2Sam 22:15; Amu 9:48Wakati Mwenyezi68:14 Mwenyezi hapa ina maana ya Shaddai kwa Kiebrania. alipowatawanya wafalme katika nchi,

ilikuwa kama theluji iliyoanguka juu ya Salmoni.

Read More of Zaburi 68