Zaburi 68:15-20
Milima ya Bashani ni milima iliyotukuka,
milima ya Bashani ina vilele vilivyochongoka.
68:16 Za 132:13, 14; 2:6; Kum 12:5Enyi milima yenye vilele vilivyochongoka,
kwa nini mnakazia macho kwa wivu,
katika mlima Mungu anaochagua kutawala,
ambako Bwana mwenyewe ataishi milele?
68:17 2Fal 2:11; Isa 66:15; Hab 3:8; Dan 7:10Magari ya Mungu ni makumi ya maelfu,
na maelfu ya maelfu;
Bwana amekuja kutoka Sinai
hadi katika patakatifu pake.
68:18 Za 47:5; 7:7; Amu 5:12; Efe 4:8; Hes 17:10Ulipopanda juu, uliteka mateka,
ukapokea vipawa kutoka kwa wanadamu,
hata kutoka kwa wale walioasi,
ili wewe, Ee Bwana Mungu, upate kuishi huko.
68:19 Za 65:5; 81:6Sifa apewe Bwana, Mungu Mwokozi wetu,
ambaye siku kwa siku hutuchukulia mizigo yetu.
68:20 1Sam 10:19; Za 56:13; Yer 45; 5; Eze 6:8Mungu wetu ni Mungu aokoaye,
Bwana Mwenyezi hutuokoa na kifo.