Zaburi 68:1-6 NEN

Zaburi 68:1-6

Zaburi 68

Wimbo Wa Taifa Wa Shangwe Kwa Ushindi

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Wimbo.

68:1 Za 89:10; 132:8; 12:5; 18:14; 92:9; 144:6; Hes 10:35; Isa 17:13; 21:15; 33:3Mungu na ainuke, watesi wake watawanyike,

adui zake na wakimbie mbele zake.

68:2 Za 37:20; 80:16; 22:14; 9:3; Hes 10:35Kama vile moshi upeperushwavyo na upepo,

vivyo hivyo uwapeperushe mbali,

kama vile nta iyeyukavyo kwenye moto,

vivyo hivyo waovu na waangamie mbele za Mungu.

68:3 Za 64:10; 97:12Bali wenye haki na wafurahi,

washangilie mbele za Mungu,

wafurahi na kushangilia.

68:4 2Sam 22:50; Za 7:17; 30:4; 66:2; 68:33; 96:2; 100:4; 135:3; 83:18; Kut 6:3; 20:21; Kum 33:26Mwimbieni Mungu, liimbieni sifa jina lake,

mtukuzeni yeye aendeshwaye juu ya mawingu:

jina lake ni Bwana,

furahini mbele zake.

68:5 Za 10:14; Kut 22:22; Kum 10:18; 26:15; Yer 25:30Baba wa yatima, mtetezi wa wajane,

ni Mungu katika makao yake matakatifu.

68:6 Lk 4:18; Za 146:7; 113:9; 102:20; 79:11; 25:16; Isa 58:11; 35:7; 49:10; 61:1Mungu huwaweka wapweke katika jamaa,

huwaongoza wafungwa wakiimba,

bali waasi huishi katika nchi kame.

Read More of Zaburi 68