Zaburi 66:13-20
66:13 Za 51:19; 22:25; 50:14; 116:14; Mhu 5:4; Yon 2:9Nitakuja hekaluni mwako na sadaka za kuteketezwa
na kukutimizia nadhiri zangu:
nadhiri ambazo midomo yangu iliahidi
na nilizotamka kwa kinywa changu
nilipokuwa katika shida.
66:15 Law 16:5; Za 51:19Nitakutolea dhabihu za wanyama wanono
na sadaka za kondoo dume,
nitakutolea mafahali na mbuzi.
66:16 Za 34:11; 71:15, 24Njooni msikilize ninyi nyote mnaomcha Mungu,
nami niwaambie aliyonitendea.
Nilimlilia kwa kinywa changu,
sifa zake zilikuwa katika ulimi wangu.
66:18 Kum 1:45; 1Sam 8:18; Yak 4:3; Isa 1:15; Ay 11:14, 15; Mit 15:29Kama ningekuwa nimeyaficha maovu moyoni mwangu,
Bwana asingekuwa amenisikiliza;
66:19 Za 18:6lakini hakika Mungu amenisikiliza
na amesikia sauti yangu katika maombi.
66:20 Za 22:24Sifa apewe Mungu,
ambaye hakulikataa ombi langu
wala kunizuilia upendo wake!