Zaburi 66:1-12 NEN

Zaburi 66:1-12

Zaburi 66

Kusifu Mungu Kwa Ajili Ya Wema Wake

Kwa mwimbishaji. Wimbo. Zaburi.

66:1 Za 81:1; 84:8; 98:4; 100:1Mpigieni Mungu kelele za shangwe, dunia yote!

66:2 Za 79:9; 86:9; Isa 42:8, 12; 43:21Imbeni utukufu wa jina lake;

mpeni sifa zake kwa utukufu!

66:3 Kum 7:21; 10:21; Za 106:22; 111:6; 18:44; 65:5; 145:6; 2Sam 22:45Mwambieni Mungu, “Jinsi gani yalivyo ya kutisha matendo yako!

Uwezo wako ni mkuu mno kiasi kwamba

adui wananyenyekea mbele zako.

66:4 Za 22:27; 7:17; 67:3Dunia yote yakusujudia,

wanakuimbia wewe sifa,

wanaliimbia sifa jina lako.”

66:5 Za 66:3; 46:8; 106:22Njooni mwone yale Mungu aliyoyatenda,

mambo ya kutisha aliyoyatenda

miongoni mwa wanadamu!

66:6 Mwa 8:1; Kut 14:21, 22; Law 23:40; Yos 3:14; Za 78:13; Isa 63:13, 14; 1Kor 10:1Alifanya bahari kuwa nchi kavu,

wakapita kati ya maji kwa miguu,

njooni, tumshangilie.

66:7 Kut 15:18; 3:16; Hes 17:10; Za 11:4; 112:10; 140:8; 145:13Yeye hutawala kwa uwezo wake milele,

macho yake huangalia mataifa yote:

waasi wasithubutu kujiinua dhidi yake.

66:8 Za 22:23Enyi mataifa, msifuni Mungu wetu,

sauti ya sifa yake isikike,

66:9 Za 30:3; Kum 32:35; Ay 12:5ameyahifadhi maisha yetu

na kuizuia miguu yetu kuteleza.

66:10 Kut 15:25; Ay 6:29; 28:1; Za 12:6; Zek 13:9Ee Mungu, wewe ulitujaribu,

ukatusafisha kama fedha.

66:11 Za 38:4; 142:7; 146:7; Isa 61:1; 10:27; 42:7, 22; Mwa 3:17; Kut 1:14Umetuingiza kwenye nyavu

na umetubebesha mizigo mizito

migongoni mwetu.

66:12 Isa 51:13; Za 18:19Uliwaruhusu watu watukalie vichwani,

tulipita kwenye moto na kwenye maji,

lakini ulituleta kwenye nchi

iliyojaa utajiri tele.

Read More of Zaburi 66