Zaburi 59:9-17
59:9 Za 18:1; 9:9; 18:2; 62:2; 71:3Ee nguvu yangu, ninakutazama wewe,
wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu,
Mungu wangu unipendaye.
Mungu atanitangulia,
naye atanifanya niwachekelee
wale wanaonisingizia.
59:11 Kum 4:9; 6:12; Za 3:3; 84:9; 89:10; 106:27; 144:6; Isa 33:3; Mwa 4:12, 13Lakini usiwaue, Ee Bwana, ngao yetu,
au sivyo watu wangu watasahau.
Katika uwezo wako wafanye watangetange
na uwashushe chini.
59:12 Za 10:7; 64:8; Mit 10:14; 12:13; Isa 2:12; 5:15; Sef 3:11Kwa ajili ya dhambi za vinywa vyao,
kwa ajili ya maneno ya midomo yao,
waache wanaswe katika kiburi chao.
Kwa ajili ya laana na uongo wanaotamka,
59:13 Za 83:18; 104:35wateketeze katika ghadhabu,
wateketeze hadi wasiwepo tena.
Ndipo itakapofahamika katika miisho ya dunia
kwamba Mungu anatawala juu ya Yakobo.
Hurudi jioni,
wakibweka kama mbwa,
wakiuzurura mji.
59:15 Ay 15:23Wanatangatanga wakitafuta chakula,
wasipotosheka hubweka kama mbwa.
59:16 Za 5:3; 88:13; 101:1; 108:1; 1Sam 2:10; 2Sam 22:3; Kum 4:30Lakini mimi nitaziimba nguvu zako,
asubuhi nitaimba juu ya upendo wako;
kwa maana wewe ndiwe ngome yangu
na kimbilio langu wakati wa shida.
59:17 Za 59:1Ee uliye Nguvu zangu, ninakuimbia sifa.
Wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu,
Mungu unipendaye.