Zaburi 57:7-11
57:7 Za 112:7; 108:1Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti;
nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
57:8 Za 33:2; 149:3; 150:3; Amu 5:12Amka, nafsi yangu!
Amka, kinubi na zeze!
Nitayaamsha mapambazuko.
Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa;
nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
57:10 Za 36:5; 108:4Kwa maana upendo wako ni mkuu, waenea hadi mbinguni,
uaminifu wako unazifikia anga.
57:11 Za 8:1; 149:3; 150:3; Amu 5:12Ee Mungu, utukuzwe juu mbinguni,
utukufu wako na uwe duniani pote.