Zaburi 57:1-6
Zaburi 57
Kuomba Msaada
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Utenzi wa Daudi. Baada ya kumponyoka Sauli pangoni.
57:1 Isa 26:20Unihurumie, Ee Mungu, unihurumie,
kwa maana nafsi yangu inakukimbilia.
Chini ya uvuli wa mbawa zako nitakimbilia
mpaka maafa yapite.
57:2 Za 138:8Namlilia Mungu Aliye Juu Sana,
Mungu atimizaye makusudi yake kwangu.
57:3 Za 18:9, 16; 69:14; 142:5, 7; 56:1; 25:10; 40:11; 115:1Hutumana kutoka mbinguni na kuniokoa,
akiwakemea wale wanaonifuatilia vikali;
Mungu huutuma upendo wake na uaminifu wake.
57:4 Za 35:17; 55:21; 64:3; Mit 30:14Niko katikati ya simba,
nimelala katikati ya wanyama wenye njaa kuu:
watu ambao meno yao ni mikuki na mishale,
ambao ndimi zao ni panga kali.
57:5 Za 108:5Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu,
utukufu wako na uenee duniani kote.
57:6 Es 6:13; Za 31:4; 9:15; 140:5; 7:15; 38:6; 10:9; 145:14; Mit 28:10; Mhu 10:8Waliitegea miguu yangu nyavu,
nikainamishwa chini na dhiki.
Wamechimba shimo katika njia yangu,
lakini wametumbukia humo wao wenyewe.