Zaburi 57:1-6 NEN

Zaburi 57:1-6

Zaburi 57

Kuomba Msaada

Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Utenzi wa Daudi. Baada ya kumponyoka Sauli pangoni.

57:1 Isa 26:20Unihurumie, Ee Mungu, unihurumie,

kwa maana nafsi yangu inakukimbilia.

Chini ya uvuli wa mbawa zako nitakimbilia

mpaka maafa yapite.

57:2 Za 138:8Namlilia Mungu Aliye Juu Sana,

Mungu atimizaye makusudi yake kwangu.

57:3 Za 18:9, 16; 69:14; 142:5, 7; 56:1; 25:10; 40:11; 115:1Hutumana kutoka mbinguni na kuniokoa,

akiwakemea wale wanaonifuatilia vikali;

Mungu huutuma upendo wake na uaminifu wake.

57:4 Za 35:17; 55:21; 64:3; Mit 30:14Niko katikati ya simba,

nimelala katikati ya wanyama wenye njaa kuu:

watu ambao meno yao ni mikuki na mishale,

ambao ndimi zao ni panga kali.

57:5 Za 108:5Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu,

utukufu wako na uenee duniani kote.

57:6 Es 6:13; Za 31:4; 9:15; 140:5; 7:15; 38:6; 10:9; 145:14; Mit 28:10; Mhu 10:8Waliitegea miguu yangu nyavu,

nikainamishwa chini na dhiki.

Wamechimba shimo katika njia yangu,

lakini wametumbukia humo wao wenyewe.

Read More of Zaburi 57