Zaburi 55:12-23 NEN

Zaburi 55:12-23

Kama aliyenitukana ni adui yangu, ningevumilia,

kama mtu mwovu angejiinua dhidi yangu,

ningejificha asinione.

55:13 2Sam 15:12Kumbe ni wewe, mwenzangu,

mshiriki na rafiki yangu wa karibu,

55:14 Mdo 1:16-17; Za 42:4ambaye awali tulifurahia ushirika mzuri,

tulipokuwa tukienda na umati hekaluni mwa Mungu.

55:15 Za 64:7; 49:14; Mit 6:5; Isa 29:5; 47:9, 11; 1The 5:3; Hes 16:30Kifo na kiwajie adui zangu ghafula,

na washuke kuzimu wangali hai,

kwa maana uovu upo ndani yao.

Lakini ninamwita Mungu,

naye Bwana huniokoa.

55:17 Za 141:2; 88:13; 92:2; 5:3; Mdo 3:1; 10:9; 10:3, 30; Lk 18:1; Dan 6:10Jioni, asubuhi na adhuhuri

ninalia kwa huzuni,

naye husikia sauti yangu.

55:18 2Nya 32:7Huniokoa nikawa salama katika vita

vilivyopangwa dhidi yangu,

ingawa watu wengi hunipinga.

55:19 Kum 33:27; Za 29:10; 78:59; 36:1; 64:4; Kut 15:18Mungu anayemiliki milele,

atawasikia na kuwaadhibu,

watu ambao hawabadilishi njia zao,

wala hawana hofu ya Mungu.

55:20 Za 7:4; 41:9Mwenzangu hushambulia rafiki zake,

naye huvunja agano lake.

55:21 Za 59:7; 57:4; 12:2; 64:3; Ufu 1:16; Mit 5:3; 6:24; 12:18Mazungumzo yake ni laini kama siagi,

hata hivyo vita vimo moyoni mwake.

Maneno yake ni mororo kuliko mafuta,

hata hivyo ni upanga mkali uliofutwa.

55:22 1Pet 5:7; Za 15:5; 18:35; 112:6; 21:7; 37:24; Mt 6:25-34Mtwike Bwana fadhaa zako,

naye atakutegemeza,

hatamwacha kamwe mwenye haki wake aanguke.

55:23 Za 5:6; 11:1; 9:15; 73:18; 94:13; 25:2; 30:3; 56:3; Isa 14:15; Eze 28:8; Lk 8:31; Ay 15:32Lakini wewe, Ee Mungu,

utawashusha waovu katika shimo la uharibifu.

Wenye kiu ya kumwaga damu na wenye hila,

hawataishi nusu ya siku zao.

Lakini mimi ninakutumaini wewe.

Read More of Zaburi 55