Zaburi 55:1-11 NEN

Zaburi 55:1-11

Zaburi 55

Maombi Ya Mtu Aliyesalitiwa Na Rafiki

Kwa mwimbishaji. Na ala za uimbaji. Utenzi wa Daudi.

55:1 Za 27:9; Mao 3:56Ee Mungu, sikiliza maombi yangu,

wala usidharau hoja yangu.

55:2 1Sam 1:15-16; Za 4:1; 77:3; 86:6-7; 142:2Nisikie na unijibu.

Mawazo yangu yananisumbua na nimehangaishwa

55:3 2Sam 16:6-8; 17:9; Za 143:3; 44:16; 71:11kwa sauti ya adui,

kwa kukaziwa macho na waovu,

kwa sababu wananiletea mateso juu yangu

na kunitukana kwa hasira zao.

55:4 Ay 18:11; Za 6:3; 102:3-5; Yn 12:27; Mt 26:37, 38; 2Kor 1:8-10Moyo wangu umejaa uchungu,

hofu ya kifo imenishambulia.

55:5 Ay 4:14; Eze 7:18; 2Kor 7:15; Isa 21:4; Kum 28:67; Yer 46:5; 49:5Woga na kutetemeka vimenizunguka,

hofu kuu imenigharikisha.

Nilisema, “Laiti ningekuwa na mbawa za njiwa!

Ningeruka niende mbali kupumzika.

55:7 1Sam 23:14Ningalitorokea mbali sana

na kukaa jangwani,

55:8 Za 31:20; 77:18; Isa 4:6; 25:4; 28:2; 29:6; 32:2ningaliharakisha kwenda mahali pa salama,

mbali na tufani kali na dhoruba.”

55:9 Mwa 4:17; 11:9; Mdo 2:4; Za 11:5; Isa 59:6; Yer 6:7; Eze 7:11; Hab 1:3Ee Bwana, uwatahayarishe waovu

na uwachanganyishie semi zao,

maana nimeona jeuri na ugomvi mjini.

55:10 1Pet 5:8Usiku na mchana wanazunguka juu ya kuta zake,

uovu na dhuluma vimo ndani yake.

55:11 Za 5:9; 10:7Nguvu za uharibifu zinatenda kazi mjini,

vitisho na uongo haviondoki mitaani mwake.

Read More of Zaburi 55