Zaburi 51:1-9
Zaburi 51
Kuomba Msamaha
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Baada ya kukemewa na nabii Nathani kwa kuzini na Bathsheba.
51:1 2Sam 24:14; 12:13; Za 39:8; 86:15; 25:7; 119:88; 9:13; Neh 4:5; 9:27; Isa 63:7; Kol 2:14; 2Nya 6:23; Mdo 3:19Ee Mungu, unihurumie,
kwa kadiri ya upendo wako usiokoma,
kwa kadiri ya huruma yako kuu,
uyafute makosa yangu.
51:2 Rum 3:3; Yer 2:22; 13:27; Mdo 22:16; Mit 20:30; Isa 4:4; Ebr 9:14; Zek 13:1; Ufu 1:5; 1Kor 6:11; Eze 13:1; 36:25; Mt 23:25, 26; 1Yn 1:7, 9Unioshe na uovu wangu wote
na unitakase dhambi yangu.
51:3 Isa 59:12; Za 32:5Kwa maana ninajua makosa yangu,
na dhambi yangu iko mbele yangu daima.
51:4 1Sam 15:24; Mwa 20:6; Lk 15:21; Rum 3:4Dhidi yako, wewe peke yako, nimetenda dhambi
na kufanya yaliyo mabaya machoni pako,
ili uthibitike kuwa wa kweli unenapo,
na kuwa na haki utoapo hukumu.
51:5 Law 5:2; Ay 5:7; 14:4; Rum 5:12; Yn 3:6Hakika mimi nilizaliwa mwenye dhambi,
mwenye dhambi tangu nilipotungwa mimba kwa mama yangu.
51:6 Ay 9:4; 34:32; Za 119:66; 143:10Hakika wewe wapendezwa na kweli itokayo moyoni,
ndani sana ya moyo wangu wanifundisha hekima.
51:7 Eze 36:25; Hes 19:6; Zek 13:1; Kut 12:22; Ebr 9:19; Isa 4:4; 1:19; 43:25; 44:22Nioshe kwa hisopo, nami nitakuwa safi,
unisafishe, nami nitakuwa mweupe kuliko theluji.
51:8 Isa 35:10; Kut 12:46; Yer 33:11; Yoe 1:16Unipe kusikia furaha na shangwe,
mifupa uliyoiponda na ifurahi.
51:9 Yer 16:17; Zek 4:10; 2Sam 12:13Ufiche uso wako usizitazame dhambi zangu,
na uufute uovu wangu wote.