Zaburi 50:16-23 NEN

Zaburi 50:16-23

50:16 Za 25:10; Isa 29:13Lakini kwake mtu mwovu, Mungu asema:

“Una haki gani kunena sheria zangu

au kuchukua agano langu midomoni mwako?

50:17 1Fal 14:9; Mit 1:22; 5:12, 13; Rum 2:21; 2The 2:10-12Unachukia mafundisho yangu

na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.

50:18 Rum 1:32; 1Tim 5:22; Ay 22:15Unapomwona mwizi, unaungana naye,

unapiga kura yako pamoja na wazinzi.

50:19 Za 10:7; 36:3; 52:2; 101:7Unakitumia kinywa chako kwa mabaya

na kuuongoza ulimi wako kwa hila.

50:20 Mt 10:21Wanena daima dhidi ya ndugu yako

na kumsingizia mwana wa mama yako.

50:21 Isa 57:11, 16; 62:1; 42:14; 64:12; 50:2; Mhu 8:11; Za 6:1; 18:15; 85:5; 76:6; 104:7; Rum 2:4Mambo haya unayafanya, nami nimekaa kimya,

ukafikiri Mimi nami ni kama wewe.

Lakini nitakukemea

na kuweka mashtaka mbele yako.

50:22 Ay 8:13; Mik 5:8; Isa 17:10; Kum 32:39“Yatafakarini haya, ninyi mnaomsahau Mungu,

ama sivyo nitawararua vipande vipande,

wala hapatakuwepo na yeyote wa kuwaokoa:

50:23 Za 85:13; 98:3; 9:14; 91:16; Isa 52:10Atoaye dhabihu za shukrani ananiheshimu mimi,

naye aiandaa njia yake

ili nimwonyeshe wokovu wa Mungu.”

Read More of Zaburi 50