Zaburi 48:1-8
Zaburi 48
Sayuni, Mji Wa Mungu
Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora.
48:1 2Sam 22:4; Mik 4:1; Yer 10:6; 31:23; Za 86:10; 96:4; 99:2; 135:5; 147:5; 46:4; 87:1; 18:3; 2:6; 1Nya 16:25; Kum 33:19; Isa 2:2; 11:9; 32:16; Zek 8:3; Oba 1:17; Dan 9:16Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana,
katika mji wa Mungu wetu,
mlima wake mtakatifu.
48:2 Isa 14:13; Za 2:6; 50:2; Mao 2:15; Eze 16:14; 20:6; Yos 13:17; Mt 5:35; Yer 3:19Ni mzuri katika kuinuka kwake juu sana,
furaha ya dunia yote.
Kama vilele vya juu sana vya Safoni48:2 Safoni inaweza ikawa na maana ya mlima mtakatifu au upande wa kaskazini. ni Mlima Sayuni,
mji wa Mfalme Mkuu.
48:3 Za 122:7; 18:2Mungu yuko katika ngome zake;
amejionyesha mwenyewe kuwa ngome yake.
48:4 2Sam 10:1-19Wakati wafalme walipounganisha nguvu,
waliposonga mbele pamoja,
48:5 Kut 15:16walimwona nao wakashangaa,
wakakimbia kwa hofu.
48:6 Ay 4:14; Mwa 3:16Kutetemeka kuliwashika huko,
maumivu kama ya mwanamke
mwenye utungu wa kuzaa.
48:7 Mwa 10:4; 41:6; 1Fal 10:22; 22:48; Eze 27:26Uliwaangamiza kama meli za Tarshishi
zilizovunjwa na upepo wa mashariki.
48:8 Yer 23:6; Mik 4:1; Zek 8:13; 14:11; Isa 2:2Kama tulivyokuwa tumesikia,
ndivyo tulivyoona
katika mji wa Bwana Mwenye Nguvu Zote,
katika mji wa Mungu wetu:
Mungu ataufanya uwe salama milele.