Zaburi 42:7-11
42:7 Eze 7:26; Mwa 1:2; 7:11; Za 69:2; Yon 2:3Kilindi huita kilindi,
katika ngurumo za maporomoko ya maji yako;
mawimbi yako yote pamoja na viwimbi
vimepita juu yangu.
42:8 Za 57:3; 16:7; 133:3; Mhu 5:18; 8:15; Kum 28:8Mchana Bwana huelekeza upendo wake,
usiku wimbo wake uko nami:
maombi kwa Mungu wa uzima wangu.
42:9 Za 18:31; 10:11; 35:14; 106:42; 9:13; 43:2; Ay 20:19Ninamwambia Mungu Mwamba wangu,
“Kwa nini umenisahau?
Kwa nini niendelee kuomboleza,
nikiwa nimeonewa na adui?”
42:10 Za 89:51; 119:42; 44:16; 6:2; 102:8; Kum 32:27Mifupa yangu inateseka kwa maumivu makali
adui zangu wanaponidhihaki,
wakiniambia mchana kutwa,
“Yuko wapi Mungu wako?”
42:11 Za 43:5Ee nafsi yangu, kwa nini unasononeka?
Kwa nini unafadhaika hivyo ndani yangu?
Weka tumaini lako kwa Mungu,
kwa sababu bado nitamsifu,
Mwokozi wangu na Mungu wangu.