Zaburi 40:9-17
40:9 Za 22:25, 31; 139:2; Yos 22:22Nimehubiri haki katika kusanyiko kubwa,
sikufunga mdomo wangu,
Ee Bwana, kama ujuavyo.
40:10 Za 89:1; 22:22; Mdo 20:20; Flp 3:9; Rum 1:16, 17Sikuficha haki yako moyoni mwangu;
ninasema juu ya uaminifu wako na wokovu wako.
Sikuficha upendo wako na kweli yako
mbele ya kusanyiko kubwa.
40:11 Zek 1:12; Za 26:3; 61:7; 43:3; Mit 20:28Ee Bwana, usizuilie huruma zako,
upendo wako na kweli yako daima vinilinde.
40:12 Za 25:17; 38:4; 65:3; 69:4; 73:26Kwa maana taabu zisizo na hesabu zimenizunguka,
dhambi zangu zimenikamata, hata nisiweze kuona.
Zimekuwa nyingi kuliko nywele za kichwa changu,
nao moyo unazimia ndani yangu.
40:13 Za 22:19; 38:22Ee Bwana, uwe radhi kuniokoa;
Ee Bwana, njoo hima unisaidie.
40:14 1Sam 20:1; Es 9:2; Za 35:26; 35:4Wote wanaotafuta kuuondoa uhai wangu,
waaibishwe na kufadhaishwa;
wote wanaotamani kuangamizwa kwangu,
warudishwe nyuma kwa aibu.
40:15 Za 35:21Wale waniambiao, “Aha! Aha!”
wafadhaishwe na iwe aibu yao.
40:16 Kum 4:29; 1Nya 28:9; Za 9:10; 119:2; 9:2; 35:27Lakini wote wakutafutao
washangilie na kukufurahia,
wale wapendao wokovu wako siku zote waseme,
“Bwana atukuzwe!”
40:17 Neh 5:19; Mk 10:21; Za 86:1; 109:22; 144:3; 20:2; 18:2; 119:60Lakini bado mimi ni maskini na mhitaji;
Bwana na anifikirie.
Wewe ndiwe msaada wangu na Mwokozi wangu;
Ee Mungu wangu, usikawie.