Zaburi 38:12-22 NEN

Zaburi 38:12-22

38:12 Za 35:4, 20; 140:5; 31:4; 141:9; 41:5Wale wanaotafuta uhai wangu

wanatega mitego yao,

wale ambao wangetaka kunidhuru

huongea juu ya maangamizi yangu;

hufanya shauri la hila mchana kutwa.

38:13 Za 115:6; 135:17; Isa 43:8; Mk 7:37Mimi ni kama mtu kiziwi, asiyeweza kusikia,

ni kama bubu, asiyeweza kufungua kinywa chake,

nimekuwa kama mtu asiyesikia,

ambaye kinywa chake hakiwezi kutoa jibu.

38:15 Za 27:14; 17:6; Yer 14:8Ee Bwana, ninakungojea wewe,

Ee Bwana Mungu wangu, utajibu.

38:16 Za 22:17; Kum 32:35Kwa kuwa nilisema, “Usiwaache wafurahie,

wala wasijitukuze juu yangu

mguu wangu unapoteleza.”

38:17 Za 37:24; 38:7; Ay 6:10Kwa maana ninakaribia kuanguka,

na maumivu yangu yananiandama siku zote.

38:18 Law 26:40; Ay 31:33; Za 32:5; Mit 28:13; 2Kor 7:9Naungama uovu wangu,

ninataabishwa na dhambi yangu.

38:19 Za 18:17; 25:19; 35:19Wengi ni wale ambao ni adui zangu hodari,

wale wanaonichukia bila sababu ni wengi.

38:20 Mwa 44:4; Yn 3:12; 1Pet 3:13; Za 54:5; 59:10; 119:23; 1Yn 3:12Wanaolipa maovu kwa wema wangu

hunisingizia ninapofuata lililo jema.

38:21 Za 22:1, 11; 27:9; 71:18; 119:8; 10:1; 35:22; 71:12Ee Bwana, usiniache,

usiwe mbali nami, Ee Mungu wangu.

38:22 Za 22:19; 40:13; 1Nya 16:35; Kut 15:2; Isa 12:2Ee Bwana Mwokozi wangu,

uje upesi kunisaidia.

Read More of Zaburi 38